Writen by
sadataley
7:48 AM
-
0
Comments
Gazeti la Charlie Hebdo kuvunja rekodi

Mistari mirefu imeshuhudiwa katika vituo vya kuuza magazeti nchini Ufaransa huku mamia ya watu wakitaka kujipatia nakala jipya la gazeti la Charlie Hebdo.
Jarida hilo limechapisha kibonzo kinachomuonyesha Mtume Muhammad akilia huku akishikilia bango linalosema ''mimi ni Charlie''.
Katika video ya dakika 12 iliyowekwa kwenye akaunti rasmi ya twitter ya wanamgambo hao wa AQAP, kiongozi wa kundi hilo anasema walipanga nani alengwe na hata kufadhili operation yote katika offisi za Charlie Hebdo.
Anasema aliyeamuru hilo kutekelezwa ni Ayman al-Zawahiri,mtu aliyemrithi marehemu Osama bin Laden aliekuwa kiongozi mkuu wa Al Qaeda .
Uhusiano kati ya kaka wawili waliofanya mashambulio hayo na AQAP ulikua tayari umebainika.
Hata hivyo ukanda huo wa video ni thibitisho kamili kwamba AQAP - ambayo Marekani wamekuwa wakiwataja kama kundi kali zaidi miongoni mwa makundi kadhaa ya wanamgambo wa kiislamu, linaweza kushambulia kwa namna ambayo wengine huenda wasiweze, licha ya kuwa halijajulikana sana kama lile kundi la Islamic state.
La kutiwa wasiwasi zaidi ni kuwa katika picha ya kanda hii ya video kiongozi huyo wa AQAP anaonekana akisimama kando ya bendera ya IS.
Chanzo: BBC
No comments
Post a Comment