Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Monday, December 22, 2014

Essebsi ajitangaza kushinda Tunisia

   
Mgombea Urais, akitangaza ushindi nchini Tunisia
Matokeo ya awali ya uchaguzi wa Rais nchini Tunisia yanaonesha kuwa Beji Caid Essebsi anaongoza kwa zaidi ya asilimia 55 ya kura
Licha ya Kujitangaza mshindi, mpinzani wake ambaye ameshika nafasi ya pili Moncef Marzouki amesema matokeo hayo yanakaribiana mno.
Wakati wafuasi wa Beji Caid Essebsi wakishangilia ushindi, kiongozi wa kampeni ya uchaguzi wa Bwana Essebsi, Mohsen Marzouk, amedai ushindi.
‘’…Kulingana na matokeo ya awali kutoka katika vituo vya kupigia kura tunaweza kusema kuwa Beji Caid Essebsi ameshinda katika duru ya pili...'' Anasema Marzouk.
Hata hivyo wakosoaji wake wanasema, ushindi wa bwana Essebsi ni ishara kurudi tena uongozi usioaminika.
Lakini mwenyewe anasema ni mtendaji ambaye ataimarisha nchi hiyo.
Uchaguzi huo unaonekana kama kilele cha mageuzi ya kisiasa ambayo nchi hiyo imepitia kufuatia machafuko ya kisiasa yaliyotokea takriban miaka minne iliyopita.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment