Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Wednesday, November 26, 2014

Tume ya Jaji Warioba yatingisha Dar


Aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba akizungumza kwenye mdahalo wa Katiba uliofanyika kwenye Ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam jana. Picha na Venance Nestory
Aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba, amesema mambo yanayotokea sasa nchini, kama viongozi kuwa na akaunti nje ya nchi na kudai ni 'vijisenti', Serikali kuingia mikataba yenye utata isiyohojiwa popote ni matokeo ya nchi kuwa na Katiba yenye maswali mengi kuliko majibu.
Akizungumza katika mdahalo wa Katiba uliokuwa na mvuto wa aina yake kwa watu kushangilia kila mjumbe aliyakuwa anazungumza ulioandaliwa na Taasisi ya Mwalimu Nyerere uliofanyika jana kwenye Ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam, Jaji Warioba huku akitumia zaidi mifano alisema mambo hayo yanaweza kuendelea kwa sababu hata Katiba Inayopendekezwa pia 'imeyabariki'.(P.T)

Katika mdahalo huo Jaji Warioba aligusia ufisadi wa Sh306 bilioni za Akaunti ya Tegeta Escrow iliyofunguliwa kwa ajili ya kuhifadhi fedha zilizokuwa zikilipwa na Shirika la Ugavi wa Umeme (Tanesco) kwa kampuni ya kufua umeme ya IPTL, kuwa ni matokeo ya kuwa na Katiba isiyo na majibu.
Huku akijinadi kuwa yeye ni mwanachama hai wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Jaji Warioba alisema kuna 'CCM imara' na 'CCM maslahi' na kwamba tabia yake ya kutoa changamoto ya masuala mbalimbali imetokana na kujengwa na Mwalimu Julius Nyerere.
Alitoa kauli hiyo baada ya kuulizwa swali na mmoja wa washiriki wa mdahalo huo kutoka Umoja wa Vijana wa CCM, Senga Abubakar aliyetaka kujua kama Jaji Warioba ataiunga mkono Katiba Inayopendekezwa, iwapo itapitishwa katika kura ya maoni.
Mdahalo huo ni wa tatu kufanywa na taasisi hiyo, baada ya ule wa pili uliofanyika katika Hoteli ya Blue Pearl Novemba 2 mwaka huu na kuvunjika kutokana na kuibuka vurugu, huku Jaji Warioba akishambuliwa alipokuwa akihitimisha hotuba yake kwa kuhoji watu wanaotumia vibaya jina la Mwalimu Julius Nyerere kupitisha hoja zao katika misingi isiyokubalika.
Tofauti na mdahalo wa pili, mdahalo wa jana ulikuwa na ulinzi mkali wa polisi na mamia ya washiriki walikaguliwa kabla ya kuingia ukumbini na kutakiwa kuandika majina ili idadi yao iweze kutambuliwa.
Katika mdahalo huo, Jaji Warioba aliambatana na waliokuwa wajumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Humphrey Polepole, Profesa Mwesiga Baregu, Joseph Butiku na Mohammed Yusufu Mshamba.
Huku akishangiliwa na mamia ya washiriki wa mdahalo huo, Jaji Warioba alisema, "Tume ya Katiba ilipendekeza miiko na kanuni za uongozi lakini Bunge Maalumu la Katiba limeyaondoa na kuyaweka katika msingi wa utawala bora.
"Hivi huwezi kuwa mzalendo na mwadilifu mpaka uwe kiongozi? Hii si misingi ya utawala bora ni misingi ya kitaifa na inamhusu kila mmoja wetu."
Alisema lengo la kuweka suala hilo ni kutaka zawadi wanazopewa viongozi ziwe za taifa, "Maana yake kama umepewa zawadi inakuwa ya taifa siyo ya kwako. Yaani kama umepewa dhamana ya uongozi na unapata 'vijisenti' viwe vya taifa."
Alisema kutokana na maoni waliyokusanya kutoka kwa wananchi na utafiti uliofanywa na Tume walibaini kuwa masuala hayo yakiwekwa katika sheria badala ya Katiba, sheria husika haitakuwa na nguvu.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment