Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Wednesday, July 30, 2014

KATIBA: Mzee Kisumo amhadharisha Rais Kikwete

Moshi. Mwanasiasa mkongwe nchini, Peter Kisumo amemtaka Rais Jakaya Kikwete na chama chake, CCM kuwa makini na msimamo Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) akisema haamini kama umoja huo umesema kila unachokusudia kukifanya.
Badala yake Kisumo alisema kinachofanywa na Ukawa ni mbinu za kujiimarisha kisiasa, jambo alilolisema iwapo CCM na Serikali yake haitakuwa makini, huenda ikaingia katika mtego na kushindwa kujinasua baada ya umoja huo kuimarika.
Kauli ya Mzee Kisumo imekuja wakati ambao viongozi wa Ukawa wameendelea kusisitiza kwamba wataendelea kususia vikao vya Bunge Maalumu la Katiba vinavyoanza mjini Dodoma, Agosti 5 mwaka huu, hadi pale madai yao yatakapozingatiwa.
Ukawa ambao unaundwa na Vyama vya Chadema, NCCR Mageuzi, CUF na baadhi ya wajumbe kutoka kundi la wajumbe 201 walioteuliwa na Rais, wanasisitiza kwamba lazima Bunge hilo lijadili Rasimu ya Katiba kama ilivyowasilishwa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba na wakitaka pendekezo la muungano wa serikali tatu lizingatiwe.
Kamati zote 12 za Bunge hilo katika maoni ya wengi zilipendekeza muundo wa Serikali mbili tofauti na uliopendekezwa katika rasimu ya Katiba iliyoandaliwa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba.
Akizungumza na gazeti hili jana, Kisumo alisema kinachotakiwa ni Ukawa kurudi bungeni wakabishane kwa hoja na kama wakishindwa, bado wenye uamuzi wa mwisho juu ya Katiba ni wananchi kwa kupiga kura ya ndio au hapana.
Awananga Z’Bar
Wakati huohuo, Kisumo alisema kuna unafiki miongoni mwa wanachama wa CCM Zanzibar ambao alisema wanasaliti kwa siri sera ya chama hicho ya muundo wa serikali mbili.
Alionyesha kushangazwa na baadhi ya wana CCM Zanzibar kupinga waziwazi sera hiyo ya CCM na kushabikia serikali tatu.
“CCM ina kamati maalumu kule Zanzibar na Tanzania Bara vilevile, lakini inaelekea kamati ile ya Zanzibar haina nguvu ya kuwabana wachache hawa wanaokiuka sera zake,” alisema Kisumo aliyepata kuwa mdhamini wa CCM kwa muda mrefu.
Kisumo alitoa mfano uamuzi wa kumvua uanachama aliyekuwa mwakilishi wa Jimbo la Kiembesamaki, Mansour Yusuph Himid kuwa haukupata uungwaji mkono Zanzibar.
“Kama sera ya CCM ni serikali mbili sasa anapotokea mtu anashabikia serikali tatu ni lazima chama kiwe na msimamo kuwa huyu siyo mwenzetu na uamuzi huo uungwe mkono,” alisema.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment