Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Monday, September 30, 2013

Makabiliano yazuka mjini Kidal, Mali

Makabiliano makali yameibuka kati ya wanajeshi wa Mali na watu wanaoshukiwa kuwa waasi katika eneo la Kidal Kaskazini mwa Mali na kusababisha hofu kuwa ghasia huenda zikakithiri.
Wapiganaji wa MNLA Kaskazini mwa Mali
Waasi hao waliwashambulia wanajeshi waliokuwa wanalinda benki mjini humo na ambao waliwafyatulia riasi.
Mkataba wa amani uliofikiwa mwezi Juni, ulikuja baada ya zaidi ya mwaka mmoja wa mapigano ambao ulisababisha jeshi la Ufaransa kuingilia kati.Wenyeji walioshuhudia tukio hilo na maafisa ambao hawakutajwa, walisema kuwa waasi kutoka kundi la Tuareg ambao walisema wanapuuzilia mbali makubaliano ya amani waliyoafikia na serikali.
Majeshi hayo yangali yanashika doria Kaskazini mwa Mali na jeshi la Mali limerejea mjini Kidal katika hali isiyoeleweka.
Mji huo ulikuwa mikononi mwa waasi wa (MNLA) kwa miezi mingi.
Gavana wa eneo hilo Adama Kamissoko aliambia shirika la habari la AFP mjini Kidal kuwa walisikia milio mingi ya risasi, na kwamba wanajeshi wa Mali walilemewa na kuondoka sehemu hiyo ingawa alisema hangeweza kuwatambua wapiganaji hao.
Hapakuwa na taarifa zozote kuhusu majeruhi kwenye makabiliano hayo.
Vurugu za Jumapili ndizo za hivi punde kutokea katika eneo hilo. Mnamo Ijumaa wanajeshi wawili walijeruhiwa mjini Kidal wakati waliporushiwa guruneti.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment