Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Monday, July 1, 2013

ZAIDI YA SHILINGI MILIONI KUMI NA SITA ZACHANGWA
Fedha hizo zimechangwa katika harambee iliyofanyika katika Usharika wa Iringa Mjini KKKT Dayosisi ya  Iringa siku ya jana 30-06-2013 lengo likiwa ni kumalizia upauaji wa Kanisa la Wilolesi.       
Akitoa taarifa ya ujenzi na  gharama zinazotakiwa Kasisi wa Kanisa Kuu Mchungaji Huruma Bimbiga alisema kuwa ili kukamilisha zoezi la upauaji jumla ya shilingi milioni kumi(10) zinatakiwa hii ni katika kukidhi mahitaji yote ikiwemo gharama za mafundi.
Baada ya  taarifa hiyo washarika na waalikwa  walisisimka na  kuanza mara moja kuchangia kazi iliyokuwa rahisi sana kwa muendeshaji wa harambee ambaye alikuwa ni  Mwenyeki wa Chama cha Mapinduzi  Madam Jeska Msambatavangu ambapo zaidi ya shilingi milioni kumi na sita  zilichangwa ili kukamilisha upauaji wa Kanisa hilo.
Akitoa shukrani baada ya harambee hiyo Msaidizi wa Askofu Mchungaji Blastone Gavile aliwashukuru washarika wote kwa kusema ni hakika wengi tumejiwekea hazina mbinguni, kwani tulilenga kupata milioni kumi lakini tumepata zaidi hivyo ninawaomba tuendelee kutoa tena na tena ili tukamilishe kazi hii iliyopo mbele yetu.
Na mwisho Msaidizi wa Askofu aliwaomba washarika na watu mbalimbali wenye mapenzi mema na kazi ya Mungu  waungane na Usharika wa Kanisa Kuu ili kukamilisha kazi hiyo kwa kuchangia.                                           
Kasisi wa Kanisa Kuu Mchungaji Huruma Bimbiga
 Hii ni sehemu ya Kanisa iliyobaki kupauliwa
                                           Muonekano wa Kanisa kwa upande wa mbele

Unaweza changia kupitia Mpesa 0756288322
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment