Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Thursday, February 25, 2016

Ugiriki yatishia EU kuhusu wahamiaji

Ugiriki imetishia kupinga maamuzi yote katika mkutano ujano wa viongozi wa Umoja wa Ulaya kuhusu uhamiaji iwapo nchi wanachama hazitakubaliana kugawana kwa uwiano wahamiaji na wakimbizi. Hatua hiyo imekuja wakati Austria na baadhi nchi za Balkani kutoa wito kupunguzwa kwa wahamiaji wanaovuka mipaka ya nchi zao. Akihutubia bunge mjini Athens Waziri Mkuu wa Ugiriki Alexis Tsipras amesema haikubaliki kwamba nchi yake iachiwe kukabiliana na tattizo hilo pekee yake. "tunachokataa kufanya ni kukubali mabadiliko katika nchi yetu kuwa ghala kubwa la nafsi za watu , na wakati huo huo tuendelee kuchukua hatua ndani ya Umoja wa Ulaya na katika mikutano ya viongozi wa Umoja huo kana kwamba hakuna jambo lolote baya. Kuanzia sasa na kuendelea Ugiriki haitakubalina na makubaliano kama hatutahakikishiwa mgawanyo wa uwiano wa mzigo na wajibu wa makazi ya wakimbizi miongoni wa nchi wanachama." Wakati huo huo mawaziri wa mambo ya ndani wa nchi 28 za Umoja wa Ulaya zinakutana mjini Brussels asubuhi hii kuzunguzia suala la tatizo la wakimbizi huku onyo likitolewa kama tatizo hilo litaendelea itakuwa vigumu kulishughulikia. Viongozi wa Umoja wa Ulaya wanatarajiwa kufanya mikutano miwili kuhusu suala la wahamiaji mwezi ujao ili kujaribu kuwa na sera kabla wimbi jingine la wahamiaji.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment