Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Saturday, August 30, 2014

David Rudisha amaliza wa tatu

Nijel Amos alimzidi nguvu David Rudisha
Katika michuano ya Diamond League ya jana usiku, Nijel Amos alimzidi kasi ya kuufukuza upepo David Rudisha katika michuano ya mita 800 mjini Zurich.
Mshindi huyo wa michuano ya Olympic David Rudisha alimaliza mbio zake katika nafasi ya tatu kwenye mbio hizo za mita 800 wakati mwanariadha mchanga na mwenye ubavu wa kutanua mapafu mbioni Nijel Amos kwa mara ingine tena amejitwalia tena ubingwa huo wa mita 800.
Na hii si mara ya kwanza kwa Amos kumshinda nguvu Rudisha kwani mwezi uliopita katika michuano ya jumuiya ya madola maarufu kama Commonwealth Games na kujitwalia medali ya dhahabu huku akitumia dakika 43. sekunde 77
Naye Ayanleh Souleiman alimshinda Rudisha na kutwaa nafasi ya pili kitendo kilichomlazimisha Rudisha kushika nafasi ya tatu.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment