Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Saturday, August 30, 2014

Okwi arejea Simba


Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba, Zacharia Hans Pope akimkabidhi jezi ya timu hiyo mshambuliaji wao mpya Emmanuel Okwi baada ya kumtambulisha jana jioni kwa waandishi wa habari. Picha na Khatimu Naheka      
Na Vicky Kimaro, MwananchiDar es Salaam. Uongozi wa Simba umemrudisha kundini mshambuliaji wake wa zamani, Emmanuel Okwi ukisema umechukua hatua hiyo: “Kumsitiri ili asipoteze kipaji chake” baada ya watani wake wa jadi Yanga, kumshtaki Shirikisho la Soka Tanzania (TFF).
Akizungumza jana, Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba, Zakaria Hans Pope alisema mbinu ambazo Yanga ilitumia Yanga kumsajili Okwi wakati alipokuwa na mgogoro na klabu ya Etoile du Sahel ya Tunisia ndiyo hiyohiyo kamati yake iliyoitumia kumrejesha Simba.
“Yanga walivyowafanyia Watunisia wakati wana mgogoro na Okwi walijiona washindi, sasa na sisi kwa mantiki hiyohiyo tumeamua kumrudisha kundini, “alisema Hans Pope.
Alisema Simba haina mkataba wowote na Okwi na kwamba anaruhusiwa kuondoka muda wowote atakapoamua huku akisema timu hiyo inasubiri uamuzi wa kesi ya mchezaji huyo na Yanga imalizike kukamilisha mchakato.
Habari zilizopatikana jana kutoka kwa baadhi ya viongozi wa Simba zinasema Okwi amemwaga wino wa kuichezea Simba kwa miaka miwili na kwamba malipo ya awali ya mkataba huo ya Dola za Marekani 10,000 alichukua mwaka jana.
Kauli ya Okwi
Akizungumzia madai yake na Yanga, Okwi alisema juzi alipewa barua na TFF ya kushtakiwa na Yanga.
Alisema katika madai, alisema Yanga inamtuhumu kuchukua fedha za usajili na kushindwa kuitumikia huku akishindwa kuipa ubingwa baada ya kufungiwa michezo minne.
“Mimi naishangaa Yanga, eti inadai fedha za usajili, usajili maana yake nisaini wa wanipe fedha, sasa hizo fedha wanazodai ni zipi? Mbona hawazungumzii mshahara wangu ambao nilikuwa nalipwa kwa kutumia nguvu, nipo tayari kukaa meza moja na Yanga katika kesi wala siogopi chochote na pale naamini kila mmoja atapata haki yake.
“Nawaomba wana Simba wanipokee mimi ni kijana wao, nitaitumikia Simba kwa moyo wangu wote, mimi ni mpya nawaahidi sitakuwa tena msumbufu,” alisema Okwi.
Wakati huo huo, baadhi ya klabu za Ligi Kuu zimelipinga Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kwa kusogeza usajili mbele mpaka leo saa 6 usiku kwa kigezo kuwa ni timu moja tu ndio iliyokuwa imekamilisha usajili wake hadi juzi saa sita usiku.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti, viongozi hao wa soka waliitaka TFF kuacha kudanganya umma wa Watanzania na badala yake iseme ukweli kilichofanya wakasogeza mbele usajili.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment