Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Thursday, May 29, 2014

Serikali yaiongezea Wizara ya Maji Sh100 bil


“Kwa sababu mmesema tusiyazungumze haya mambo kule bungeni, basi tusubiri taarifa ya uchunguzi na mimi nawaambia kama wapo wanaohusika humu ndani nakuambieni ripoti ikija hapatatosha.” Kangi Lugola 
Na Daniel Mjema na Sharon Sauwa, Mwananchi

Dodoma. Kuna kila dalili kwamba homa ya makadirio ya matumizi ya Wizara ya Maji na ile ya Nishati na Madini inazidi kupanda na jana wabunge wa CCM walikutana kwa dharura ili kunusuru bajeti hizo.
Habari kutoka ndani ya kikao hicho zinasema, Waziri Mkuu Mizengo Pinda aliwatangazia wabunge hao kuwa Serikali imekubali kuiongezea Wizara ya Maji Sh100 bilioni kufidia pengo la Mwaka wa Fedha 2013/2014.
Kadhalika wabunge hao waliambiwa kuwa Serikali pia imekubali kutoa Sh50 bilioni kwenda Wakala wa Umeme Vijijini (Rea) ambazo zilikusanywa na Hazina lakini hazikupelekwa kama taratibu zinavyoelekeza.
Taarifa za uhakika kutoka Hazina, zinaonyesha kuwa katika Mwaka wa Fedha 2013/2014, Rea ilipaswa kupokea Sh123.7 bilioni lakini hadi kufikia Machi mwaka huu, ilikuwa imepokea Sh79 bilioni. Kama ilivyokuwa katika bajeti ya Maji, kitendo cha Hazina kutoipatia Rea fedha hizo kwa wakati kuliibua hasira za wabunge wengi ambao walijipanga kukwamisha Bajeti ya Wizara ya Nishati na Madini.
Kwa upande wa Maji, katika Mwaka wa Fedha wa 2013/2014, Wizara ya Maji ilikuwa ipewe Sh184 bilioni kutekeleza miradi ya maji lakini hadi kufikia Machi mwaka huu, Serikali ilikuwa imetoa Sh86 bilioni.
Habari za uhakika zilizolifikia gazeti hili zinasema kuwa kutolewa kwa fedha hizo ambazo awali ilionekana zisingetolewa, kulitokana na jitihada kubwa zilizofanywa na Kamati ya Bunge ya Bajeti inayoongozwa na Mbunge wa Bariadi Magharibi, Andrew Chenge.
Naibu Waziri wa Fedha, Mwigulu Nchemba alikiri kwamba wizara hizo zitapatiwa fedha hizo lakini akasema siyo nyongeza bali ni utekelezaji utoaji wa fedha za mwaka 2013/2014.
“Maji tutawapa kama bilioni 50 hivi na Rea pia tutawapa kiasi kama hicho na kwa upande wa Rea tutakuwa tumetoa fedha zote kwa asilimia 100 ila Maji watapata fedha zote kabla ya kuisha kwa mwaka fedha,”alisema.
Serikali kwa Mwaka wa Fedha wa 2013/2014 ina upungufu wa Sh1.8 trilioni za bajeti ya maendeleo hali iliyosababisha baadhi ya wizara kupata asilimia kati ya 19 na 30 ya fedha za maendeleo.
Fedha za escrow
Habari zaidi zinasema ndani ya kikao hicho kuliibuka sakata la kashfa ya Sh200 bilioni ya Akaunti ya Escrow ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT) ambapo baadhi ya wabunge walitaka Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo awajibike.
Hata hivyo, Mbunge wa Mwibara, Kangi Lugola ndiye aliyemwokoa Profesa Muhongo baada ya kusema kwa vile suala hilo tayari limekabidhiwa vyombo vya kiuchunguzi, ni vyema wabunge wakasubiri ripoti hiyo.
Kwa habari ziadi ingiahttp://www.mwananchi.co.tz/habari/Kitaifa/Serikali-yaiongezea-Wizara-ya-Maji-Sh100-bil/-/1597296/2329942/-/10r1pn0z/-/index.html
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment