Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Thursday, May 29, 2014

Membe aikaribisha Takukuru wizarani


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe.PICHA|MAKTABA 
Na Daniel Mjema, Mwananchi
Dodoma. Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe amesema ataipa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) jukumu la kuchunguza ufisadi wa mamilioni ya fedha katika ununuzi wa tiketi za safari za nje za wizara yake.
Ahadi hiyo ilitokana na tishio la Mbunge wa Ole, Rajab Mbaruku la kutishia kuondoa shilingi endapo Waziri Membe asingetoa mkakati wa kupambana na ufisadi huo ulioibuliwa kwenye taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) ambayo ilifichua ununuzi wa tiketi kwa bei ya juu zaidi ya mara 16 ya bei halisi ya soko.
Katika taarifa yake alibaini ukiukwaji wa sheria za ununuzi na kwamba tiketi 56 zilizotakiwa kununuliwa kwa Sh700.9 milioni, zilinunuliwa kwa Sh974.5 milioni ikiwa ni ongezeko la Sh273.6. milioni jambo ambalo ni kinyume cha mikataba ya Mawakala wa Huduma za Manunuzi (GPSA).
CAG pia alibaini kuwa katika tiketi 22 zilizochukuliwa zikiwakilisha safari 239 za maofisa wa wizara, zilionyesha kuwa tiketi hizo zilitozwa zaidi ya kiwango kilichokubaliwa.
Juzi, Mbaruku ambaye ni mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC), alimbana Waziri Membe akitaka atoe ahadi ya jinsi wizara yake itakavyoshughulikia suala hilo na asipofanya hivyo, angeondoa shilingi kwenye mshahara wake, hatua ambayo ingesababisha kukwama bajeti hiyo.
Hata hivyo, katika majibu yake Waziri Membe alijikita zaidi katika kutetea misafara ya Rais, baada ya wabunge kulalamikia kuwa inatumia fedha nyingi za serikali kwa kuwa inakuwa na watu wengi, jibu ambalo halikumlidhisha Mbaruku.
“Sijaridhika na majibu ya waziri amejielekeza zaidi kwenye safari za Rais. Nilichokizungumza mimi ni kuzingatia kanuni za ununuzi wa umma kwamba inakiukwa,” alisema Mbaruku.
“Pia nimetoa mifano miwili ya safari ambazo zimefanywa na maofisa wake na hazikuwa za kushtukiza ambazo zimetumia fedha nyingi tofauti na zile zilizotakiwa kutumiwa katika uhalisia wake.”
“Kwa hiyo bado nashikilia shilingi ya mshahara wa waziri hadi atoe commitment (hakikisho) namna ya kushughulikia ufisadi unaofanywa na maofisa wake.”
Ndipo Membe aliposema: “Mimi nilikuwa nataka tu nimshauri mwenzangu... kwa kuwa ni kitu specific cha watu... Kwa nini asitupe muda sisi twende tukalifanyie kazi kwa sababu siyo jambo kubwa.
“Siyo suala la sera ni watu mafisadi kama anavyowaita. Wako mle, tutakwenda kuchunguza na tutaomba wenzetu wa Takukuru waliangalie halafu mambo yakienda vizuri nitaleta taarifa hapa bungeni,” alisema.
Kauli ya Membe ilionekana kumgusa Naibu Spika, Job Ndugai, ambaye alimsihi Mbaruku alichukue jambo hilo ili likashughulikiwe na kamati za Bunge hasa ikizingatiwa yeye ni mwenyekiti wa LAAC.
Kwa habari ziadi ingia http://www.mwananchi.co.tz/habari/Kitaifa/Membe-aikaribisha-Takukuru-wizarani/-/1597296/2329916/-/wnc526z/-/index.html
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment