Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Friday, May 30, 2014

Prof Tibaijuka asalimu amri Kigamboni


Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka.PICHA|MAKTABA 
Dar es Salaam. Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka juzi aliwekwa kitimoto na wabunge waliotishia kuondoa shilingi kukwamisha bajeti ya wizara yake kiasi cha kumlazimisha Waziri Mkuu Mizengo Pinda kuingilia kati na kuokoa jahazi.
Pinda aliokoa jahazi baada ya mbunge wa Kigamboni, Dk faustine Ndungulile kukataa kurudisha shilingi akieleza kuwa Serikali haijashirikisha wadau katika mradi huo utakaogharimu Sh11.7 trilioni utakapokamilika.
“Nimeona kuna tatizo la elimu kwa umma kuhusu mradi huu na ushirikishwaji,” alisema Pinda baada ya mbunge wa viti maalum (CCM), Esther Bulaya kumuomba aingilie kati ili kuondoa aibu kwa Serikali.
“Serikali tunaomba tuachiwe suala hili. Wizara itaanza kutoa elimu kuhusu mradi huu.”
Awali Tibaijuka, ambaye alikuwa na kazi ya kujibu tuhuma za ufisadi wa kutumia madaraka vibaya katika mgogoro wa Chasimba na kiwanda cha saruji cha Wazo Hill jijini Dar es salaa, alijitahidi kupangua hoja za kambi ya upinzani na wakati mwingine kumshambulia mbunge wa Kawe, Halima Mdee aliyeshikia bango mgogoro wa wananchi wa Chasimba na kiwanda cha saruji cha Wazo Hill.
Tibaijuka, ambaye alikuwa mkurugenzi wa Shirika la Makazi ya Umoja wa Mataifa (UN-Habitat), baadaye alisema anakubaliana na mawazo ya wengi kuhusu hali na mazingira ya mji wa Kigamboni uliopo jijini Dar es Salaam hivyo kwa kuwa kuna kasoro na kwamba suala la ushirikishwaji linawezekana.
Sakata hilo, ambalo lilionekana kumnyima raha Waziri Tibaijuka kadri mjadala ulivyokuwa unaendelea, lilitokea wakati Bunge lilipokaa kama kamati kupitisha vifungu vya bajeti hiyo ya Sh88.9 bilioni.
Mbunge wa Kigamboni, Dk Ndungulile aliondoa shilingi katika mshahara wa waziri akipinga namna Serikali inavyoutekeleza mradi wa uendelezaji wa wa mji wa Kigamboni bila ya kuwashirikisha wakazi wa Kigamboni.
Dk Ndungulile alisema kuwa wananchi hawashirikishwi katika mradi huo wala hawaelewi hatima ya malipo ya fidia ya nyumba zao.
Badala yake, mbunge huyo alisema, wananchi wanalazimishwa kununua hisa kwa ajili ya umiliki wa mradi huo, kitu ambacho alikipinga.
“Suala la kuwa na hisa si la lazima ni hiari, kwanza waziri anazidi kuwachanganya wananchi wa Kigamboni ambao hawajaelimishwa kuhusu suala hilo, hivyo naondoa shilingi katika bajeti yako,” alisema Dk Ndungulile.
Mbunge huyo aliungwa mkono na wabunge wengine akiwamo mbunge wa viti maalum (CCM), Esther Bulaya, mbunge wa Temeke, Zuberi Mtemvu na mbunge wa viti maalumu (CCM), Zarina Madabida.
Kwa habari zaidi ingiahttp://www.mwananchi.co.tz/habari/Kitaifa/Prof-Tibaijuka-asalimu-amri-Kigamboni/-/1597296/2331324/-/fdskv8z/-/index.html
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment