Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Friday, May 30, 2014

Mawaziri acheni jeuri, ubabe kuweni wasikivu

Kwa muda mrefu sasa, serikali imekuwa ikijinadi kuwa ni sikivu kwa matatizo ya wananchi wake.
Hiyo imetokea kuwa kaulimbiu muhimu kwa viongozi wake wengi kwa ngazi mbalimbali, wakiwamo mawaziri kila wanapozungumzia masuala mazito ya jamii.
Kwa kutumia kaulimbiu hiyo, mara nyingi Serikali imekuwa ikijinadi kuwa ipo makini, inawatumikia wananchi au Watanzania wote kwa umakini na uadilifu.
Lakini, kwa kuangalia majadiliano na mijadala mingi ambayo imekuwa ikiendelea ndani ya Bunge la Jamhuri ya Muungano linaloendelea na vikao vyake mjini Dodoma, usikivu huu wa Serikali kwa hakika unatia shaka.
Tunasema kauli hizi zinatia shaka hasa kwa sababu inaonekana maoni na ushauri unaoonekana kuwa mzuri na wenye tija unaotolewa bungeni, umekuwa hautiliwi maanani na wakati mwingine kubezwa na hata kufanyiwa mzaha.
Ushauri huo ambao hutolewa ama na wabunge au kupitia maoni ya kamati za Bunge na mawaziri kivuli wa kambi ya upinzani, umekuwa ukitolewa majibu mepesi na pengine kubinafsishwa na matokeo yake yamekuwa ni kushambuliwa kwa msemaji au mtoaji ushauri.
Hii imetokea karibu katika wizara zote zilizowasilisha hotuba zao za makadirio ya mapato na matumizi kwa mwaka 2014/15.
Mawaziri hao walitumia muda mwingi kushambulia kambi ya upinzani, wasemaji wao na kutotolea majibu mapungufu ambayo yalibainishwa na kamati husika za wizara hizo.
Matukio ya hivi karibuni ni yale yaliyomuhisisha Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa na Wizara wa Maliasili na Utalii ambao walitumia muda mwingi kushambulia maoni au hoja za wabunge, hasa wa upinzani, na hivyo kutotoa majibu yanayolenga kuondoa utata kwenye masuala yaliyohojiwa.
Hatutaki kuamini kuwa maoni, maswali na hoja zinazotolewa dhidi ya serikali zote si sahihi na zinastahili kubezwa na kutolewa majibu yasiyoondoa utata unaotakiwa uwekwe bayana.
Mawaziri na Serikali hawana budi kutambua kuwa wabunge ni wawakilishi wa wananchi na mambo wanayohoji wanafanya kwa niaba ya wananchi na huweza kuhoji kwa sababu wanatumia muda wao mwingi kufanya tafiti kwa ajili ya kupata uwezo wa kuihoji na kuisimamia serikali.
Kwa hiyo, tunadhani Serikali haina budi kujitazama upya jinsi inavyopokea na kufanyia kazi ushauri na maswali yanayoibuliwa na wabunge.
Kwa habari zaidi ingiaMawaziri acheni jeuri, ubabe kuweni wasikivu
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment