Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Monday, March 31, 2014

Bunge la Katiba kuanza kazi rasmi leo

Wabunge wakiwa Bungeni mjini Dodoma 
Na Mussa Juma, Mwananchi
Dodoma. Wakati Bunge la Katiba leo linaanza kujadili sura mbili za Rasimu ya Katiba ambazo zitalenga Muundo wa Muungano, Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) umewataka wajumbe wake kutokuondoka Dodoma hadi kumaliza kujadili sura hizo.
Kwa mujibu wa ratiba ya Bunge iliyotangazwa Ijumaa iliyopita na makamu mwenyekiti wa Bunge hilo, Samia Saluhu, leo wajumbe wataanza kujadili sura ya Kwanza ya Rasimu ambayo inahusu Jina, mipaka, alama, lugha na Tunu za Taifa.
Sura ya sita, inahusu muundo wa Muungano, vyombo vya utendaji na mamlaka ya Serikali, nchi washirika na uhusiano wa nchi washirika.
Katibu wa Bunge la Katiba, Yahya Hamis Hamad alisema utaratibu wa kujadili rasimu kwa kuanza na sura hizo umetolewa na Kamati ya Uongozi kwa kuzingatia kanuni ya 58 ya Bunge la Katiba.
Kanuni hiyo ya 58 (3) inasema kamati ya uongozi itakuwa na majukumu ambayo ni “(a) kujadili na kuamua mambo yote yanayohusu uendeshaji bora wa shughuli za BungeMaalumu na kamati zake.
“(b) kujadili na kupanga ratiba ya utekelezaji wa shughuli za Bunge na (c) kujadili na kufanya uamuzi kuhusu masuala yatakayohitaji usuluhishi na maridhiano”.
Tamko la Ukawa
Mjumbe wa Bunge hilo, John Mnyika akizungumza kwa niaba ya Mwenyekiti wa Ukawa, Freeman Mbowe, alisema kuanzia leo Bunge litaanza kujadili muundo wa Muungano ambao alisema ndiyo moyo ya Rasimu ya Katiba hivyo wajumbe wote wa Ukawa watashiriki.
“Tumewaomba wajumbe kutokuondoka wakati wa kujadili sura hizi mbili kwani ndiyo roho ya rasimu na tunaonya ikifikia hatua CCM wakachakachua, tutachukua maamuzi (uamuzi) mazito na kwa gharama zozote,” alisema Mnyika.
Mnyika alisema tayari wamepata taarifa kuwa wajumbe kutoka CCM wataingia na mapendekezo yao na yatapigiwa kura kwa kujua wao wapo wengi pamoja na uteuzi wa wajumbe 201 walioteuliwa na Rais Jakaya Kikwete .
Hata hivyo alisema wakati wa kupitisha vifungu vya rasimu hiyo ni wazi kuwa CCM haina theluthi mbili kwa Zanzibar na kama wakipeleka mapendekezo ya kutaka kuvunja sheria na kanuni kwa masilahi yao hawatakubali.
Mnyika alisema licha ya Mwenyekiti wa Kamati ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba kueleza upungufu wa mfumo wa Serikali mbili na hivyo kupendekeza Serikali tatu ambayo ni maoni ya wananchi, bado CCM inashinikiza na kutetea msimamo wao.
Mnyika alionyesha waraka aliodai wa siri wa CCM kuhusu jinsi ya kupinga mapendekezo ya Sura ya Kwanza na ya sita katika rasimu hiyo.
Alionya kwa mujibu wa sheria ya mabadiliko ya kupitisha sura katika rasimu, ni lazima ipatikane theluthi mbili kwa upande wa Tanzania Bara na kwa Zanzibar.
Tamko hilo la Ukawa limekuja siku chache baada ya wajumbe wake kadhaa, akiwapo Mbunge wa Jimbo la Arusha, Godbless Lema kutangaza nia ya kuondoka Dodoma, akipinga mwenendo wa Bunge hilo hasa upigaji wa kura za wazi na siri kwa wakati mmoja.
Lema alidai kwa mazingira yaliyojengwa bungeni amepoteza imani ya kupatikana kwa Katiba ya wananchi.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment