Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Monday, March 31, 2014

Israel:Ehud Olmert alipokea hongo

Waziri Mkuu wa zamani wa Israel, Ehud Olmert amepatikana na hatia ya kupokea hongo.
Ehud Olmert ana kosa la kupokea hongo katika sakata inayohusu kipande cha ardhi
Mahakama moja ya Mji wa Tel Aviv alimpata na hatia kiongozi huyo wa zamani katika ksahfa iliyotokea wakati akiwa Meya wa mji huo mkuu.
Kadhalika Mahakama imesema kesi hiyo imefichua utawala uliokuwa fisadi na ambao uliendeleza ufisadi mkubwa katika kipindi cha miaka mingi.Inaarifiwa hongo ilitolewa na kupokelewa katika uuzaji wa kipande cha ardhi ili kuharakisha ujenzi wa nyumba za kifahari.
Sakata hiyo iliyojuliakana kama 'Holy Land' iliyohusisha kipande cha ardhi mjini Tel Aviv ilipelekea Bw. Olmert mwenye umri wa miaka 68 kujiuzulu kama Waziri MKuu mwaka 2008.
Hii ndio mara ya kwanza Waziri Mkuu wa Israel amepatikana na hatia ya Hongo. Duru zinasema kuwa hukumu hii huenda ikawa mwisho wa ndoto ya kisiasa ya bw. Olmert.
Kwa muda mrefu Olmert alikana kufanya makosa yoyote na pia tuhuma sawa na hii dhidi yake zilitupiliwa mbali na mahakama mbali mbali.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment