Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Friday, January 31, 2014

35 wauawa CAR mapigano yakichacha

Kamati ya kimataifa ya msalaba mwekundu imesema kuwa watu 35 wameuawa katika mji mkuu wa Jamhuri ya Afrika ya Kati, Bangui katika kipindi cha siku tatu zilizopita.
Rais mpya wa muda nchini CAR, Catherine Samba Panza
Msemaji wa kamati hiyo ya Red Cross mjini Bnagui ,Nadia Dibsy,amesema kuwa mji huo sasa unakumbwa na vita vibaya.
Vita inasemekana vimekithiri huku wanajeshi 1,600 wa Ufaransa na wengine 5,000 wa Muungano wa Afrika wakiwa nchini humo kujaribu kutuliza hali.Kwa mujibu wa shirika la habari la Associated Press, miili ilionekana ikiwa imekatakatwa kwa mapanga na kutapakaa kote.
Mgogoro wa kisiasa ulianza mwezi Machi mwaka jana kutokana na mapinduzi ya kijeshi yaliyotokea wakati huo ambapo waasi waisilamu walimsaidia aliyekua Rais Djotodia kuingia mamlakani kwa nguvu.
Tangu hapo vita vimekuwa vikichacha kati ya waasi waisilamu na wakristo.
Na sasa kwa kuwa waisilamu wameondoka mamlakani, wakristo nao wameanza kulipiza kisasi.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment