Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Monday, December 30, 2013

HUYU NDIO BINTI WA MAREHEMU ANGELA CHIBALONZA, MUNGU ANAMTUNZA


Picha ya juu binti wa aliyekuwa nyota wa muziki wa injili Afrika mashariki na kati marehemu Angela Chibalonza, bintiye wa pekee baby Wonder ambaye muonekano wake anafanana na mama yake ingawa GK haijajua kama atafuata nyayo za mama yake ama Mungu amempa talanta nyingine.

Picha hii ni kutoka kwa mama yake wa kufikia ama mlezi ambaye ni mke wa mtume Elisha Muliri ambaye ndiye alikuwa mume wa hayati Angela Chibalonza. Angela bado anakumbukwa na ataendelea kukumbukwa kutokana na alama kubwa aliyoacha kupitia uimbaji wake katika kumtangaza Kristo  kupitia album zake mbalimbali.

Hapa Baby wonder akiwa na mama yake mdogo Tete Meshak mdogo wa Angela Chibalonza ambaye pia ni mwimbaji kama alivyokuwa dada yake. Picha ni mali ya Tete.

Hebu tumalizie mwaka kwa kusikiliza wimbo huu "Wewe ni mwema" kutoka kwake marehemu Angela Chibalonza Muliri kati ya nyimbo ambazo zinabariki kuzisikiliza kutokana na sauti, upako na mpangilio wa vyombo kwa ujumla bila kusahau maneno yake. Barikiwa
Habarina Gospel Kitaa
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment