Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Monday, December 30, 2013

Nchi ya Urusi yaendelea kukumbwa na mashambulizi na kusababisha vifo vya watu

Mlipuko kwenye kituo che reli mjini Volgograd,umegharimu maisha ya zaidi ya watu kumi

Na RFI
Watu zaidi ya kumi wamekufa na wengine zaidi ya thelathini wamejeruhiwa katika shambulizi la bomu kwenye kituo cha treni mjini Volgograd kusini magharibi mwa nchi ya Urusi. Tuko hilo limetokea, baada ya tukio lingine liliotokea jana jumapili kwenye kituo cha mjini kilichoko karibu na mji wa Caucase, na kugharimu maisha ya watu 17.

Idara ya uchunguzi nchini humo imesema shambulizi hilo limetekelezwa na mtu aliyejitoa mhanga anayeaminika kuwa ni mwanamke aliyejilipua baada ya kuwaona polisi wa ukaguzi.
Serikali ya Urusi imeimarisha usalama katika vituo vya mabasi, reli na viwanja vya ndege ili kukabiliana na mashambulizi zaidi, ambayo yanazidisha hofu ya usalama katika michuano ya Olimpiki ya Sochi inayotarajiwa kuanza nchini humo majuma sita yajayo.
Kamati ya uchunguzi wa tukio hilo imesema katika ripoti yake kwamba mshambuliaji wa kujitowa Muhanga alikuwa ni mwanamke na tayari uchunguzi umeanzishwa ili kubaini tukio hilo la Kigaidi.
Mashahida wa tukio hilo wamesema mshambuliaji huyo alijilipua katika eneo ambako kulikuwa na watu wengi wakiwemo polisi wa Usalama.
Duru za kitabibu zimearifu kuwa watu kumi na sita wamepoteza maisha wengine takriban 45 wamejeruhiwa wakiwemo watoto.
Rais wa Urusi Vladimir Poutine amevitaka vyombo vya dola na vile vya sheria kufanya kila liwezekanalo ili kubaini wahusika wa tukio hilo na kuwafikisha mbele ya vyombo vya sheria.
Ulinzi na usalama vimeimarishwa zaidi baada ya tukio hilo katika vituo mbalimbali vya treni na kwenye viwanja vya ndege nchini humo.
Umoja wa Mataifa na vikosi vya kujihami vya nchi za magharibi Nato wamelaani vikali shambulio hilo ambalo katibu mkuu wa Nato Anders Fogh Rasmussen amesema halina sababu yoyote.
 
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment