Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Monday, December 30, 2013

HOLLYWOOD KUMTANGAZA YESU MWAKA 2014, MACHO YAELEKEZWA HUKO


Mwaka 2014 unatajwa kama mwaka wa udhihirisho na ukamilisho, hili linaungwa mkono na wasanii maarufu wa filamu duniani kutoka mji wa Hollywood maarufu kwa kutengeneza sinema kwani mwaka 2014 wanatarajia kuachia sinema kutoka katika Biblia. Kati ya sinema hizo ni pamoja na NOAH wakiigiza mambo ya gharika watu waliyoipata kwakutomtii Mungu na nabii wake aliyepewa maelezo ambaye kwakiswahili tunamwita Nuhu. Waigizaji wanaotarajiwa kung'ara katika sinema hiyo ni pamoja na Russell Crowe, Anthony Hopkins, Emma Watson, na Jennifer Connelly. Sinema hii itatoka wakati wa pasaka 2014, mpaka sasa kuna malumbano makubwa katika mtandao wa YouTube kuhusu ukweli wa jambo hili kutokea miaka ya nyuma hususani kwa watu wasioamini.

Sinema nyingine inayotarajiwa kutoka 2014 ni pamoja na filamu kumhusu nabii Moses ama Musa kutoka katika kitabu cha Kutoka ndani ya Biblia takatifu ambapo filamu hii itaonyesha zaidi maisha ya Moses ambayo hayajawahi kuonyeshwa ama kuigizwa katika sinema ikiwa pamoja na uhusiano wake na Farao na watu waliokuwa wakimzunguka kwahiyo itakuwa kitu cha tofauti chini ya muongozaji wake ama director Ridley Scott waigizaji wakuu wakiwa ni Christian Bale, Joel Edgerton, Aaron Paul, Ben Kingsley, na Sigourney Weaver. Sinema hii inatarajiwa kutoka Disemba 2014.

Nyingine ni "Son of God" au mwana wa Mungu kwa kiswahili ambayo imeigizwa kwa mtindo wa tamthilia ikiwa na masaa 10. Ni maisha ya Yesu kuzaliwa, kukua, kufanya kazi, kukamatwa na kusulubiwa na wayahudi kisha kufufuka, filamu hii itakuwa sawa na filamu nyingine inayoitwa "The Bible" ambayo imejaribu kuigiza habari ya Biblia chini ya Mark Burnett pamoja na Roma Downey huku mwigizaji mkuu akiwa Diogo Morgado. Inatarajiwa kuanza kuonyeshwa katika majumba ya sinema mwezi february 2014.

Sinema nyingine inayosubiriwa kwa hamu ni "Day of War" siku ya vita ikiwa ni sinema iliyotumia mamilioni ya pesa kutengenezwa ikielezea vita ya Mfalme Daudi kama ilivyoandikwa na Cliff Graham kupitia mwendelezo wa vitabu vyake vya "Lion of war"lakini ikichukua zaidi kilichoandikwa kwenye Biblia hasa vita ya mfalme Daudi na Goliath. Lakini bado haijafahamika lini filamu hiyo itazinduliwa ndani ya mwaka 2014.

Wakati hayo yakijiri Hollywood watu mbalimbali wameonekana kuvutiwa na mambo yatakayojili mwaka 2014 ikionyesha wazi kwa watu wanaomwamini Mungu kupokea mengi kutoka kwake kutokana na kuwa mwaka wa utimilifu. Lakini watu hao wamekuwa wakimuomba Mungu kwamba sinema hizo zisiwe za kufurahisha watu tu bali zilete maana na ukombozi kwa watu watakaozitazama. Katika historia ya Hollywood inaonyesha kati ya filamu zilizoleta pesa nyingi ama kupendwa ni filamu zilizotokana na habari za Biblia kama "Passion of Christ" ilikuwa ya mafanikio tele nyingine ni "The Prince of Egypt" chini ya Line Cinema na nyinginezo.

Kaa mkao wa kula mdau wa GK, wewe kama ni mwanamaombi zidisha maombi zaidi, kama wewe ndio mtenda dhambi ndio wakutenda zaidi lakini yote katika yote kila mtu atavuna alichopanda. Siku njema.

Habari kwa hisani ya Blog ya Gospel Kitaa
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment