Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Thursday, September 5, 2013

HABARI PICHA ZA KUMUAGA KULOLA, VIONGOZI MBALIMBALI WAMSINDIKIZA

Zifuatazo ni baadhi ya picha za matukio ya maazishi ya Askofu Mkuu wa EAGT, Dakta Moses Kulola, ambaye amezikwa kwenye uwanja wa kanisa la EAGT Bugando jijini Mwanza. Gospel Kitaa itakueletea picha zote za kilichojiri. Endelea kutembelea.
Rais Kikwete akisaini kitabu cha maombolezo, akipokelewa na makamu askofu mkuu, Mwaisabila.
Mke wa Rais, Mama Salma Kikwete akiweka sahihi kitabu cha maombolezo mara baada ya kuwasili eneo la maazishi, EAGT Bugando.


Maaskofu wa EAGT wakijiandaa kushusha jeneza kwenye kaburi.
Maaskofu wa EAGT wakiteremsha jeneza lililobeba mwili wa Askofu Mkuu Moses Kulola kwenye kaburi. Udongoni amerudi.
Mjukuu mmojawapo akiwa ameshikilia bango lenye picha ya marehemu.
Rais Jakaya Kikwete akitoa salamu za rambiwambi.
Wafiwa wakifuatilia 'vituko' vya Masanja

Baada ya kifo ni hukumu, sio kesi, asema Masanja

Emanuel Mgaya, almaarufu Masanja Mkandamizaji akisalimiana na baadhi ya wageni mara baada ya kuhudumu.

Florah Mbasha na wajukuu wenzake wakiimba kwa huzuni.
Mchungaji Abiudi Misholi akiimba wimbo aliotunga takriban nusu saa mara baada ya kupata taarifa za msiba wa Askofu Kulola.
Nyota imezimika, anaimba mchungaji Abiudi Misholi
Sehemu ya wageni waliohudhuria, Askofu Bruno Mwakibolwa wa EAGT Mito ya Baraka akiratibu baadhi ya mambo kwa simu.

Mtoto akikwea mti upande wa pili wa ukuta, ili kushuhudia namna shughuli yote inavyoenda ya kumuaga Askofu Kulola.
A living proof
Askofu wa BCIC, Sylvester Gamanywa akiweka shada la maua kwenye kaburi la Askofu Moses Kulola.
Waziri mkuu aliyepita, Edward Lowasa akiweka shada la maua kwenye kaburi la Askofu Moses Kulola

Makamu Askofu MKuu wa EAGT, Mwaisabila akiweka shada la maua kuhitimisha zoezi, kisha mafundi wakachukua nafasi yao.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment