Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Wednesday, February 28, 2018

Magari ya Dizeli yapigwa marufuku Ujerumani


Teknolojia inazidi kukua ulimwenguni kote kila siku ikiwa ni matokeo ya kuvumbuliwa kwa vitu, mifumo, vifaa na vitu vingine vipya ambavyo ni vya teknolojia za juu zaidi kuliko vilivyopo.

Kutoka nchini Ujerumani, miji ya nchi hiyo itaanza kupiga marufuku magari ya zamani yanayotumia dizeli, hii ni kufuatia maagizo mapya ya Mahakama.

Mahakama ya Utawala ya Shirikisho huko Leipzig imesema kuwa miji ya Stuttgart na Duesseldorf ya nchini humo inaweza kupiga marufuku magari ya zamani zaidi na ambayo yanaharibu mazingira katika maeneo yaliyoathirika na uchafuzi wa mazingira.

Uamuzi huo uliofanywa na mahakama hiyo umekuja baada ya majimbo ya Ujerumani kukata rufaa inayopinga utekelezwaji huo ambao tayari ilikuwa unafanywa na mahakama hizo za mwanzo za Stuttgart na Duesseldorf.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment