Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Thursday, January 26, 2017

Rais wa Marekani Donald Trump ametia saini agizo hili

Rais wa Marekani Donald Trump ametia saini agizo linaloidhinisha kuanza kujengwa ukuta katika mpaka wa Marekani na Mexico.

Agizo hilo ni mojawapo ya ahadi za Rais Trump wakati wa kampeni ambapo aliazimia kujenga ukuta wa zaidi ya kilomita 3,000 kuitenganisha Marekani na Mexico kwa lengo la kudhibiti wahamiaji kutoka Mexico kwa madai kuwa wanachangia kuleta matatizo mengi nchini Marekani yakiwemo ya dawa za kulevya, uhalifu na ubakaji.

Amesisitiza kuwa gharama ya ujenzi wa ukuta huo italipwa na Mexico, suala ambalo hata hivyo Rais wa Mexico imelipinga vikali na kuapa kutolipa fedha yeyote.
Bunge la Marekani litahitaji kuidhinisha agizo hilo la Rais Trump kabla ya utekelezaji. Wakati huo huo Rais Trump alitarajiwakukutana na Rais wa Mexico ikulu ya ya Marekani mwishoni mwa mwezi huu.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment