Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Monday, December 5, 2016

Majivu ya mwili wa Fidel Castro yazikwa Santiago, Cuba

Majivu ya mwili wa Fidel uliochomwa yasafirishwa katika maziko mjini Santiago

Image captionMajivu ya mwili wa Fidel uliochomwa yasafirishwa katika maziko mjini Santiago
Majivu ya aliyekuwa rais wa Cuba Fidel Castro yamezikwa katika kiunga cha makaburi mjini Santiago, na hivyo kumaliza siku tisa za maombolezo ya kitaifa nchini Cuba.
Familia na wageni wachache walialikwa katika shughuli hiyo ya faragha, iliyofanywa karibu na makumbusho ya shujaa wa uhuru wa Cuba, Jose Marti.
Hapo jana, rais wa Cuba, Raul Castro, amesema serikali yake itakataza barabara au eneo lolote kupewa jina la Fidel, na ndivyo Fidel mwenyewe alivyoagiza.
Mbele ya mhadhara mkubwa mjini Santiago, alisema Fidel Castro hakutaka kufanywa kama kiongozi wa madhehebu.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment