Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Thursday, February 25, 2016

Upinzani nchini Uganda wasisitiza kupinga matokeo

Sheria ya uchaguzi ya Uganda inatoa siku 10 za kuasilisha malalamishi kuanzia siku ya kutangazwa matokeo. Chama kiku cha upinzani nchini Uganda kimesema kinafanya kila kiwezalo kutafuta ushahidi utakaopelekea kupinga matokeo ya uchaguzi uliofanyika Februari 18. Sheria ya uchaguzi ya Uganda inatoa siku 10 za kuasilisha malalamishi kuanzia siku ya kutangazwa matokeo. Mwenyekiti wa chama cha upinzani cha FDC Mugisha Muntu amesema chama chake kinafanya kila juhudi ili kuwasilisha ushahidi kabla ya wakati uliowekwa kumalizika. Hata hivyo ameongeza kuwa kumekuwa na dhuluma na ukandamizaji kutoka kwenye vyombo vya usalama vya serikali ikiwemo idara ya polisi. Muntu ameyasema haya kufuatia kukamatwa mara kadhaa kwa Dkt Kizza Besigye aliekuwa mgombea urais wa chama cha FDC. Mwenyekiti wa tume ya uchaguzi Badru Kiggundu alimtangaza rais Yoweri Museveni kuwa mshindi kwa kujipatia asilimia 60.07 ya kura zilizopigwa huku Besigye akifuatia kwa asilimia 35.37 za kura.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment