Writen by
sadataley
8:18 PM
-
0
Comments
Luhaga Mpina
Mbunge huyo wa Kisesa ameahidi kukuza uchumi kwa kuongeza misingi ya upatikanaji wa fedha. Kuongeza mapato ya nchi na kuyasimamia kwa manufaa ya nchi na wananchi kwa ujumla.
Lazaro Nyalandu
Waziri wa Maliasili na Utalii ameahidi kujenga uchumi imara utakaosaidia kupunguza ukali wa umaskini kwa wananchi na kuwawezesha wananchi mmojammoja kupata kipato kulingana na shughuli anazofanya.
Dk Augustine Mahiga
Balozi huyo mkongwe ameahidi kuongeza kipato cha kati cha wananchi, kukuza uchumi kwa kupambana na umaskini kwa kutoa msukumo katika kilimo, viwanda, uchukuzi na utalii.
Dk Mwele Malecela
Mtaalamu huyo wa masuala ya tiba ameahidi kuhakikisha huduma za afya zinapatikana kwa watu wote, kutoa elimu ya ufundi ili kuongeza ajira kwa vijana, msukumo mkubwa ukiwa kukuza uchumi.
Elidephonce Bihole
Ameahidi kuwapeleka Watanzania katika nchi ya ahadi, kuinua uchumi wa nchi kwa kutumia rasilimali zilizopo.
Dk Hassy Kitine
Amepania kuirudisha Tanzania ya Mwalimu Julius Nyerere, kuwa na sera sahihi za maendeleo ya nchi, kuinua kilimo, viwanda, uchukuzi, afya, elimu na kuinua maisha ya kila mwananchi.
Subscribe to:
Post Comments
(
Atom
)
No comments
Post a Comment