Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Wednesday, July 1, 2015

kivumbi urais part 3

Waziri Mkuu, ameahidi kuanzia pale Serikali ya Awamu ya Nne itakapoishia akisema yanayoonekana sasa ni matunda ya CCM. “Nikiingia nimepanga kuongeza ukuaji wa uchumi wa pamoja ili kuondoa wigo kati ya mwenye nacho na asiyekuwa nacho.” William Ngeleja Mbunge wa Sengerema amesema atapambana na maadui sita ambao ni maradhi, umaskini, ujinga, maradhi, rushwa, ufisadi na kukuza maadili. Benard Membe Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa ameahidi kusimamia utawala bora kwa kuhakikisha kila mmoja anawajibika katika nafasi yake kwa uadilifu na kuzingatia sheria za nchi. Pia atasimamia utawala bora, elimu na maendeleo ya jamii. Peter Nyalali Ameahidi kukuza demokrasia, kuleta mabadiliko katika nyanja mbalimbali zikiwamo za uchumi, jamii, michezo, nishati, utawala bora na kuimarisha upatikanaji wa ajira kwa vijana na kusimamia usalama wa Taifa. January Makamba Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia ameahidi kuinadi Ilani ya CCM na kuunda baraza dogo la watu 18, waadilifu na wachapakazi. Dk Khamis Kigwangalla Mbunge wa Nzega atapambana na rushwa ikiwa ni pamoja na kuichukia, kukuza ajira, kubana matumizi kuwezesha wajasiriamali kupambana na umasikini.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment