Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Wednesday, July 1, 2015

kivumbi part 5

Dk Asha-Rose Migiro Waziri huyo wa Katiba na Sheria ameahidi kutekeleza Ilani ya CCM kuendelea kukuza uchumi utakaowafikia wananchi walio wengi zaidi. Joseph Chagama Ameahidi kupambana na tatizo la ajira kwa vijana. Kusimamia utekelezaji wa Sheria , uadilifu na elimu. Balozi Ali Karume Mwanadiplomasia huyo ameahidi kuwapo kwa uhuru bila kujali dini, itikadi za vyama, elimu wala vyeo, kupambana kukuza kilimo kwanza na elimu baadaye anasema ni ngumu kusoma kama una njaa. Makongoro Nyerere Mbunge wa Afrika Mashariki anasema vipaumbele vyake vitatokana na ilani ya CCM. Maliki Malupu Ataboresha elimu, kilimo kwa kuwa na mbegu bora kuongeza msukumo katika kilimo chenye tija na kumwezesha mkulima mdogo kujikimu. Dk Ghalib Bilal Makamu wa Rais atasimamia uwajibikaji katika sekta ya umma, kulinda haki za binadamu na kuongoza kwa misingi ya sheria. Pia, kusimamia matumizi mazuri ya rasilimali za Taifa na kuboresha usimamizi wa mapato.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment