Writen by
sadataley
8:20 PM
-
0
Comments
Amos Siyantemi
Atadumisha amani, kurudisha mfumo wa mabalozi wa nyumba 10, kuwafilisi mali wote watakaokamatwa na rushwa.
Dk John Magufuli
Waziri wa Ujenzi ameahidi kutekeleza kwa nguvu zote ilani ya CCM.
Jaji Augustino Ramadhani
Ameahidi kuyaangalia mapendekezo ya wananchi yaliyoachwa kwenye Katiba Inayopendekezwa na kuyatafutia dawa mapema matatizo yakiwamo ya rushwa, ufisadi na tatizo la mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi.
Dk Mussa Kalokola
Amesema atakomesha unyanyasaji wanaofanyiwa Watanzania na kurejesha mfumo utakaoleta mchangamko wa uchumi, ambao unadorora kwa kukosekana uongozi bora.
Ritta Ngowi
Atakuza uchumi, kujenga kituo cha kulea kuwahudumia wastaafu, walemavu na wasiojiweza.
Monica Mbega
Atatekeleza ilani ya CCM na kuendeleza mazuri yaliyofanywa na waliotangulia.
Nicholas Mulenda
Atahakikisha CCM inakuwa imara zaidi.
Banda Sonoko
Ameahidi kuvaa viatu vya Mwalimu Nyerere kwa kusimamia nchi kujiendesha kwa kodi za nchi na kufufua uchumi wa viwanda.
Helen Elinawinga
Atapambana na adhabu za vifo kwa viongozi.
Dk Harrison Mwakyembe
Atatekeleza ilani ya CCM, kupambana na rushwa kwa nguvu zote.
Mathias Chikawe
Ataendeleza mapambano dhidi ya ujinga, maradhi na umaskini na kupiga vita ufisadi.
Antony Chalamila
Ameguswa kuwatumikia wananchi.
Subscribe to:
Post Comments
(
Atom
)
No comments
Post a Comment