Writen by
sadataley
10:53 AM
-
0
Comments
Shirikisho la soka la Ivory
Coast limesema kuwa huenda likasusia mechi ya kufuzu kwa dimba la
mabingwa barani Afrika dhidi ya wapinzani wao Sierra Leone ikihofia
kuenea kwa Ebola.
Mchuano huo ambao umeratibiwa kuchezwa mjini
Abidjan tarehe 6 Septemba umeibua taharuki miongoni mwa maafisa wa Afya
na serikali kuu inatishia kuipiga marufuku.Hofu hiyo inatokana na kuenea kwa homa ya Ebola katikamataifa 5 kanda ya Afrika Magharibi ikiwemo Sierra.
Tayari Sierra Leone imetaja kikosi cha wachezaji wanaocheza nje ya Sierra Leone ilikuepusha hatari ya kueneza Ebola Ivory Coast .
Sierra Leone imeagiza maafisa wote wa ukufunzi kufanyiwa uchunguzi wa kutosha kabla ya kuingia Ivory Coast .
Hadi kufikia sasa haijulikani iwapo CAF itaichukulia hatua zaidi Ivory Coast iwapo itasusia kuchuana na Sierra Leone au itaruhusiwa kuendelea na mechi za kufuzu.
No comments
Post a Comment