Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Wednesday, July 2, 2014

MATUKIO MAKUBWA YAKUHDUHURIA KWA MKAZI WA DAR ES SALAAM JUMAPILI HII


Wapenzi wa muziki wa injili nchini hususani wakaao ndani ya jiji la Dar es salaam na vitongoji vyake watapata fursa ya kuhudhuria matukio makubwa mawili jumapili hii yanayotarajiwa kufanywa na kati ya kwaya kongwe nchini ambazo uimbaji wake umekuwa ukiwabariki wengi kwa miaka mingi.
Siku hiyo ya jumapili ya tarehe 6 Julai kwaya ya Uinjilisti Sayuni kutoka usharika wa Kilutheri Kinondoni inatarajiwa kuweka wakfu DVD yake ya tatu iitwayo 'Dua na Maombezi' katika ibada mbili zitakazofanyika kanisani kwao Kinondoni na kufuatiwa na tamasha la uimbaji majira ya mchana mara baada ya kuisha kwa ibada ya pili, ikisindikizwa na Beatrice Moses, Amkeni, Fellowship Kinondoni pamoja na wana wa Gusa AIC Chang'ombe.
Kwaya hiyo ambayo moja ya sifa zake ni kuimba live na kwaustadi zaidi wakiimba kwa kumtukuza Mungu, wamekuwa katika mazoezi ya kuhakikisha siku ya jumapili wanaimba kwa viwango zaidi lakini kubwa zaidi ni kuona watu watakaofika wanakutana na uwepo wa Mungu katika uzinduzi huo ambao makamu wa Askofu wa Dayosisi ya mashariki na pwani kanisa la Kilutheri George Fupe pamoja na mkewe wanatrajiwa kuungana na kwaya hiyo katika tendo hilo.
Kwaya ya Sayuni inafahamika vyema kwahuduma yake kwa wanafunzi wa Ukwata kwa miaka mingi, lakini pia ndio kwaya ya kwanza kutoa album za mapambio ambazo zilitokea kupendwa zikiwemo Yawe Yawe au Bwana wa mabwana, parapanda italia, Simba wa Yuda, Bwana Yesu anakuja, Safari na nyimbo nyinginezo. Mwenyekiti wa kwaya hiyo bwana James Makatta amewataka wapenzi wa muziki wa injili kutokosa siku ya jumapili kwakuwa itakuwa siku ya kukumbukwa kwa watakaohudhuria.
Aidha tukio lingine siku ya jumapili ni kwaya ya Neema Gospel kutoka kanisa la AIC(T) pastorate ya Chang'ombe jijini Dar es salaam ambao wamekuwa gumzo siku za karibuni kutokana na mabadiliko ya uimbaji wao, wanatarajia kuachia album yao iitwayo 'Haki yake Mungu' ambayo imebeba nyimbo nyingine ambazo zimetokea kupendwa sana kila wanapokwenda kwenye mwaliko hususani kwenye ibada za kusifu na kuabudu katika kanisa la Dar es salaam Pentecoste Kinondoni (DPC). 
Kwaya hiyo ambayo ni kongwe imetokea kupendwa toka enzi hizo walipotoa video yao ya kwanza 'Dunia imeoza' ikiwa na nyimbo mablimbali kama sinyinyi mlionichagua ulioimbwa na solo matata wa kwaya hiyo mwanadada Tabitha lakini kama haitoshi kwaya hiyo pia ambayo ndiyo aliyokuwa akiimbia marehemu Steven Kanumba kabla hajaanza kuigiza walitoa video ya pili inayoitwa 'Pengine Hukujua' na kufuatiwa na vieo ya tatu inayopendwa mpaka leo iitwayo 'Kuna mamba kivukoni'.
Neema Gospel Choir wanatarajiwa kusindikizwa na waimbaji kama AIC Dar es salaam Choir kutoka Magomeni, John Lisu na timu yake pamoja na kwaya maarufu kutoka hapo hapo kanisani chang'ombe iitwayo AIC Chang'ombe wana wa Gusa ambao pia wameahidi kufika katika uzinduzi wa kwaya ya Sayuni Kinondoni siku hiyo ya jumapili. Matukio yote mawili hayatakuwa na kiingilio chochote bali ni bure.
Habari na Gospel Kitaa
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment