Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Monday, June 16, 2014

Ufaransa yaanza kwa kishindo

Mshambuliaji wa Ufaransa, Karim Benzema (katikati) akipiga shuti ambalo liligonga mwamba na kipa wa Honduras, Luis Lopez (kushoto) akajifunga wakati akijaribu kuzuia shuti hilo hivyo kuipatia Ufaransa bao la pili katika mechi ya kundi E ya Fainali za Kombe la Dunia kwenye Uwanja wa Beira-Rio mjini Porto Alegre jana. Ufaransa ilishinda 3-0. Picha na AFP.   
Porto Alegre, Brazil. Ufaransa imeanza vyema Fainali za Kombe la Dunia baada ya kuichapa Honduras mabao 3-0 kwenye Uwanja wa Beira-Rio mjini Porto Alegre, Brazil na kuongoza kundi E.
Katika dakika ya 43, Ufaransa ilipata penalti baada ya Wilson Palacios kumsukuma Paul Pogba kwenye eneo la hatari na mwamuzi kumpa kadi ya pili ya njano Palacios na kadi nyekundu.
Mshambuliaji Karim Benzema alipiga penalti hiyo na kuipatia Ufaransa bao la kwanza kabla ya dakika ya 48 kipa Noel Valladares kujifunga akijaribu kuzuia shuti la Benzema na hivyo Ufaransa kupata bao la pili.
Kama hiyo haitoshi, dakika ya 72, Benzema aliipatia Ufaransa bao la tatu kwa shuti kali baada ya shuti la Mathieu Debuchy kuzuiliwa. Hivi sasa Ufaransa inaongoza kundi E ikifuatiwa na Uswisi, Ecuador na Honduras.
Katika mechi ya awali, Uswisi iliibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Ecuador katika mechi iliyochezwa kwenye Uwanja wa Nacional Mane Garrincha mjini Brasilia. Mechi hiyo ambayo ilihudhuriwa na mashabiki 68,351, Ecuador ndiyo iliyokuwa ya kwanza kupata bao katika dakika ya 22 lililofungwa na Enner Valencia kwa kichwa akiunganisha mpira wa faulo uliopigwa na Walter Ayovi, lakini Uswisi walisawazisha bao hilo katika dakika ya 48 mfungaji akiwa Admir Mehmedi kwa kichwa akiunganisha mpira wa kona uliopigwa na Ricardo Rodriguez.
Mechi ikiwa inaonekana itamalizika kwa sare, Haris Seferovic akiwa ametokea benchi aliipatia Uswisi bao la pili katika dakika ya 90+3 akiunganisha mpira wa kona uliopigwa na Rodriguez.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment