Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Monday, June 16, 2014

Casillas, Del Bosque wabeba mzigo


Kipa wa Hispania, Iker Casillas (kulia) akijinamia huku mshambuliaji wa Uholanzi, Arjen Robben (katikati) na kiungo Wesley Sneijder wakishangilia baada ya Robben kufunga bao la tano wakati wa mchezo uliozikutanisha timu hizo Fonte Nova, Salvador. Picha zote na AFP 
Salvador, Brazil. Kipa na nahodha wa Hispania, Iker Casillas alipotea kabisa, Gerard Pique alizidiwa mbio na Sergio Ramos alifanya uzembe wa hali ya juu.
Nini kilichoikuta ngome ya Hispania ambayo kwa kawaida inasifika kwa umakini?
Ngome hiyo ya Hispania ndiyo iliwasaidia kunyakua mataji matatu makubwa mfululizo, lakini Ijumaa ilikuwa tofauti baada ya kuruhusu mabao 5-1 kutoka kwa Uholanzi, hicho kikiwa ni kipigo cha kwanza kikubwa kwa mabingwa hao watetezi wa dunia tangu walipofungwa namna hiyo mwaka 1950.
‘’Sijui ni neno gani zuri la kuelezea hiki kilichotukuta,’’ alisema kocha Vicente del Bosque. ‘’Sitaki kumlaumu yeyote. Kufungwa kwa timu hakuwezi kuwa sababu ya mtu mmoja. Sitaki kumnyooshea kidole (Casillas) au yeyote.’’
Casillas alitoa zawadi ya bao la pili la Robin van Persie wakati kipa huyo wa Real Madrid alipoteleza kabla ya kupigwa chenga na Arjen Robben aliyefunga bao la tano.
“Nilishindwa kufanya vitu vile nilivyozoea, hasa katika mchezo huu wa ufunguzi wa Kombe la Dunia,’’ alisema Casillas. “Haikuwa siku yangu nzuri, sikuwa kwenye kiwango changu cha kawaida. Nakubali kupokea lawama zote.’’
Pique alipitwa kirahisi na Robben alipofunga bao la kwanza na pia alizidiwa mbio na Mdachi huyo alipofunga bao la pili.
“Kipindi cha pili kilikuwa kibaya zaidi kwetu,’’ alisema Pique. “Tulipotea kabisa mchezoni.’’
Katika mchezo mmoja, Hispania imeruhusu mabao mengi kuliko magoli waliyofungwa kwenye fainali mbili walizochukua ubingwa.
Mara ya mwisho kupokea kipigo cha aina hii ilikuwa katika fainali za mwaka 1950 zilizofanyika Brazil, na Hispania walinyukwa 6-1 na wenyeji Brazil.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment