Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Tuesday, April 29, 2014

Nape abeza Ukawa kuungana

Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa, Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye.PICHA|MAKTABA 
Na Raymond Kaminyoge, Mwananchi
Dar es Salaam. Siku moja baada ya vyama vya upinzani vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) kutangaza kusimamisha mgombea mmoja katika nafasi ya urais na ubunge majimboni, CCM kimebeza hatua hiyo kikisema viongozi hao hawawezi kukaa zizi moja.
Akizungumza jana, Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa, Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye alisema viongozi wa Ukawa ni genge la wasaka madaraka hivyo hawawezi kuungana kwa hilo.
Nnauye alisema viongozi wa vyama vya upinzani waliungana kwa lengo la kutafuta Katiba bora, lakini wamebadilisha ajenda na sasa wanazungumzia urais mwaka 2015.
“Hawa kumbe ni waongo, malengo yao siyo Katiba, bali ni kutafuta madaraka, muungano wa kutafuta madaraka hauwezi kufanikiwa kwa sababu viongozi wote wa Ukawa ni wapenda madaraka,” alisema Nnauye.
Alisema wananchi watashuhudia umoja huo ukisambaratika kwa sababu viongozi wa Ukawa hawawezi kuvumiliana na kuachiana madaraka.
“Kuungana ni jambo zuri, lakini sababu za kuungana zinapotajwa kuwa ni kumsimamisha mgombea mmoja wa urais mwaka 2015, watasambaratika kabla ya muda huo kufika,” alisema.
Alisema Ukawa wamewadanganya wananchi kwamba wanasimamia Katiba bora kumbe ajenda kuu ni kuongoza nchi.
Gazeti hili jana liliripoti kuwa Ukawa pia wanataka kusimamisha mgombea mmoja wa ubunge katika kila jimbo la uchaguzi.
Katika habari hiyo, Mwenyekiti wa Chadema ambaye pia ni Kiongozi wa Kambi ya Rasmi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba na Mwenyekiti wa NCCR Mageuzi, James Mbatia walikiri kuwapo mpango huo.
Taarifa za kuwapo mpango, zimekuja siku chache tangu kufichuliwa kwa mpango mwingine wa kuundwa upya kwa Baraza la Mawaziri Kivuli ambalo litawajumuisha wabunge wa vyama vya upinzani katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika mkutano wa bajeti unaoanza Mei 6, mwaka huu.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment