Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Sunday, April 27, 2014

JWTZ wadaiwa kutembeza kipigo, wajeruhi

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi wa Kinondoni, Camilius Wambura.PICHA|MAKTABA 
Na Kalunde Jamal, Mwananchi
Wakazi wawili wa eneo la Kiluvya Gogoni, Wilaya ya Kinondoni Mkoa wa Dar es Salaam, Barnabas Swai (33), Pendo Mchaki (26) na Lugano Kalinga, wamejeruhiwa kutokana na kipigo cha watu wanaodaiwa kuwa ni askari wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania, (JWT) na mmoja wao akilazwa katika Hospitali ya Mwananyamala.
Tukio hilo lilitokea juzi na inadaiwa kuwa chanzo cha kipigo hicho ni mmoja wa maofisa wa jeshi hilo aliyefika kwenye baa na mkewe na baadaye ulizuka ugomvi uliodaiwa kuzuka kutokana na mke wa ofisa huyo kudhulumiwa nyama choma, lakini walizidiwa nguvu na kupigwa.
Habari zinasema baada ya tafrani kutokea ofisa huyo wa jeshi aliondoka, baadaye walifika askari na kuanza kupiga watu ovyo njiani, kwenye maduka na baa za eneo hilo na kujeruhi baadhi ya watu.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi wa Kinondoni, Camilius Wambura jana aliliambia gazeti hili kuwa hajapata taarifa za tukio hilo.
“Ofisini kwangu sina taarifa kama hiyo, nashukuru kwa kunifahamisha nitazifanyia kazi,” alisema Wambura. Msemaji wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ), Luteni Kanali Eric Komba hakupatikana kuzungumzia tukio hilo, baada ya simu yake kutokuwa hewani.
Barnabas inaelezwa amepata majeraha katika maeneo mbalimbali ya mwili na damu imevujia kwenye mapafu, wakati Pendo ambaye ni mkewe alipatiwa matibabu katika Hospitali ya Tumbi na kuruhusiwa.
Hata hivyo, akizungumza kwa shida kutokana na maumivu katika Wodi namba 5A, Hospitali ya Mwananyamala alikolazwa, Swai alisimulia kwamba yeye na mkewe walikuwa kwenye Baa ya Gogoni Inn na waliona watu wanakimbia ovyo eneo hilo na nao walipoamua kukimbia, walivamiwa na wanaodhania kuwa ni askari wa JWTZ kutokana na kuvaa suruali za jeshi na mashati ya kiraia.
Alisema kuwa walipigwa kwa kutumia mikanda ya jeshi iliyokuwa na vyuma, virungu na vitu vya ncha kali na wakati akipigwa alitobolewa eneo la mgongoni na kupata maumivu makali huku akipumua kwa shida.
Hivyo yeye na majeruhi wengine walipelekwa Hospitali ya Tumbi Kibaha kabla ya kuhamishiwa Mwananyamala.
“Walinifanyia upasuaji na kuniweka mpira wa kutoa damu iliyoanza kuganda, lakini kwa sasa naendelea vizuri, ingawa nahisi maumivu makali sehemu ya mgongoni,” alisema Swai huku akiomba apatiwe dawa ya maumivu kutokana na maumivu makali anayoyahisi.
Daktari wa zamu katika wodi namba 5A, katika Hospitali ya Mwananyama Daktari Brian Minja alisema: “Kulingana na faili lake, ‘mgonjwa huyo alipokewa usiku na daktari mwingine, inaonyesha alikuwa na tatizo la kupumua kutokana na damu kuvujia kwenye mapafu. Karibu lita mbili za damu ilitolewa.”
Naye Upendo Swai alisema kwamba mume wake aliumizwa kwa sababu alikuwa akimkinga yeye kuzuia asipigwe zaidi na askari hao na kufafanua kwamba katika kipigo hicho, yeye aliumizwa usoni kwa kukanyagwa na viatu pamoja na kuchomwa na kitu chenye ncha kali eneo la kwapani.
Kwa upande wake Lugano Kalinga ambaye ni mkazi wa eneo hilo, alisema alipigwa na askari hao, ingawa alifanikiwa kukimbia na hakupata majeraha makubwa.
Alisema kilichosababisha wapate kipigo hicho ni ofisa mmoja wa jeshi kugombana na muuza chipsi baada ya kukataa kumlipa fedha zake, ndipo kijana huyo alipigana na ofisa huyo pamoja na mkewe lakini aliwazidi nguvu.
“Baada ya kutoka pale, ndiyo maaskari wakavamia eneo hilo na kuanza kumpiga kila waliyemwona, hali inayoonekana ni kupata maelekezo kutoka kwa huyo ofisa aliyepigana kwenye baa ya Kiluvya, ”alisema Kalinga.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment