Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Friday, January 31, 2014

Bandari bubu tatu kutambuliwa rasmi

Tanga. Mkoa wa Tanga upo kwenye mchakato wa kurasimisha bandari bubu tatu ili zipandishwe hadhi na kufanya kazi chini uangalizi wake, tofauti na sasa zinatumika kupitisha biashara za magendo na wahamiaji haramu.
Akizungumza na Kamati ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Mazingira juzi, Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Chiku Gallawa alisema bandari hizo bubu zinatumika vibaya, hivyo ni bora zikatambuliwa ili kuingiza mapato serikalini.
Gallawa alitaja bandari hizo kuwa ni Jasini iliyopo wilaya ya Mkinga, Kigombe wilayani Muheza na Kipumbwi iliyopo Pangani na kwamba, hizo ni kati ya 40 zilizopo Tanga.
Alisema baada ya kuzitembelea na kukagua shughuli zinazofanyika kila siku, Serikali imebaini bandari hizo bubu zinavusha bidhaa mbalimbali. Pia, zinatumika kama milango ya kuingia kutoka maeneo mbalimbali duniani.
Mwenyeikiti wa kamati hiyo, James Lembeli alipongeza Mkoa kwa kuchukua hatua hiyo, kwani siku zilizopita zilikamatwa meno ya tembo nje ya nchi na kubainika kuwa zimepitia mkoani hapa.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment