Writen by
sadataley
12:24 PM
-
0
Comments
Serikali ya DRCongo imesema watu sabini wamepoteza maisha wakiwemo wanajeshi watatu katika tukio hilo na jeshi limefaanikiwa kutuliza ghasia hizo zilizo shuhudiwa kwenye maeneo tofauti ya jiji ukiwemo uwanja wa ndege, kituo cha Radio na Runinga ya taifa pamoja na eneo la makao makuu ya jeshi.
Vurugu hizo zilianzia katika mji mkuu Kinshasa ambapo kundi la vijana waliokuwa na silaha za jadi ambao walikiteka kituo cha runinga ya taifa RTNC wakati kikiperusha matangazo yake moja kw amoja huku waandishi wa habari wawili wakashuhudiwa moja kwa moja wakifanyiwa vitisho na vijana hao wa Pasta Joseph Mukungubila ambaye aliwahi kuwania urais mwaka 2006 na kwa sasa anajiita kuwa nabii wa bwana.
Msemaji wa serikali ya DRCongo Lambert Mende amesema jeshi la serikali linadhibiti hali ya mambo, na kwamba uchunguzi umeanzishwa ili kubaini viongozi walionyuma ya vijana hao waasi.
Ghasia kama hizo zimeshuhudiwa pia katika miji ya Kindu na Lubumbashi na kusababisha kukatishwa kwa shughuli za usafiri wa kimataifa kwenye uwanja wa ndege wa Njili. Akizungumza na RFI idhaa ya Kifaransa pasta Joseph Mukungubila Mutombo amesema wafuasi wake hawakuwa na silaha.
Vurugu hizo zilianzia katika mji mkuu Kinshasa ambapo kundi la vijana waliokuwa na silaha za jadi ambao walikiteka kituo cha runinga ya taifa RTNC wakati kikiperusha matangazo yake moja kw amoja huku waandishi wa habari wawili wakashuhudiwa moja kwa moja wakifanyiwa vitisho na vijana hao wa Pasta Joseph Mukungubila ambaye aliwahi kuwania urais mwaka 2006 na kwa sasa anajiita kuwa nabii wa bwana.
Msemaji wa serikali ya DRCongo Lambert Mende amesema jeshi la serikali linadhibiti hali ya mambo, na kwamba uchunguzi umeanzishwa ili kubaini viongozi walionyuma ya vijana hao waasi.
Ghasia kama hizo zimeshuhudiwa pia katika miji ya Kindu na Lubumbashi na kusababisha kukatishwa kwa shughuli za usafiri wa kimataifa kwenye uwanja wa ndege wa Njili. Akizungumza na RFI idhaa ya Kifaransa pasta Joseph Mukungubila Mutombo amesema wafuasi wake hawakuwa na silaha.
No comments
Post a Comment