Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Monday, October 7, 2013

Ghasia Mombasa baada ya Sheikh kuuawa

Mmoja wa walionusurika baada ya Sheikh Ibrahim Ismael na wengine watatu kuuawa  Mombasa, Kenya, Oct. 3, 2013.
Mmoja wa walionusurika baada ya Sheikh Ibrahim Ismael na wengine watatu kuuawa Mombasa, Kenya, Oct. 3, 2013.

Waandamanaji  katika mji wa Mombasa Kenya, wamechoma Kanisa moja  na magurudumu ya magari Ijumaa baada ya watu wenye silaha kumpiga risasi Alhamis jioni na kumuuwa kiongozi mmoja maarufu wa ki-Islam na washirika wake watatu.
 
Ghasia zilizuka Ijumaa siku moja baada ya washambuliaji wasiofahamika kumfyatulia risasi Sheikh Ibrahim Rogo na washirika wake wakati wakisafiri ndani ya gari moja karibu na Mombasa.
 
Mashahidi wanasema polisi walifyatua gesi ya kutoa machozi  na kuingia katika mapambano na vijana wa ki-islam katika  kitongoji kimoja cha Mombasa.
 
Shirika la Msalaba Mwekundu la Kenya linasema mtu mmoja alifyatuliwa risasi na kuuwawa wakati wa ghasia hizo.Sheikh Ibrahim Rogo alionekana kama mrithi wa  Sheikh Aboud Rogo Mohammed, ambaye alihubiri kwenye msikiti huo huo mjini Mombasa na alishutumiwa kuwa na uhusiano na wanamgambo wa ki-Islam wa al-Shabab.
 
Ghasia zilizuka baada ya Rogo kuuwawa kwa kupigwa risasi  Agosti 27 mwaka 2012 katika barabara hiyo hiyo ambayo  pia Sheikh Ibrahim aliuwawa Ijumaa.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment