Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Sunday, September 8, 2013

Tokyo yasherehekea kutuzwa Olimpiki 2020

Tokyo imekuwa ikisherehekea kuchaguliwa kuwa mwenyeji wa michezo ya Olimpiki ya mwaka wa 2020.
Watoto wanaoneshana habari za magazeti kuwa Tokyo imechaguliwa kuandaa 2020 Olympics
Mji mkuu wa Japan uliishinda kwa urahisi miji ya Istanbul na Madrid.
Tokyo ni mji wa tano ambao utakuwa umeandaa Olimpiki mara mbili.Tangazo hilo lilotolewa na rais anayeondoka wa kamati ya kimataifa ya michezo ya Olympiki Jacques Rogge lilishangiliwa sana mjini Tokyo.
Mwandishi wa BBC amesema kuwa mji huo ulijitembeza vyema katika siku ya mwisho ya kampeni lakini piya ulionekana kuwa thabiti kifedha na kiusalama
Waziri Mkuu wa Japan, Shinzo Abe, aliiambia kamati ya Olimpiki, IOC, kwamba matatizo ya miyonzi ya nuklia katika kinu cha nishati cha Fukushima hayataathiri michezo mjini Tokyo.
Imewekwa na Happy Adam
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment