Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Sunday, September 8, 2013

Kerry atafuta kuungwa mkono

Waziri wa mashauri ya nchi za nje wa Marekani, John Kerry, anakutana na mawaziri wa Jumuia ya Nchi za Kiarabu mjini Paris, akiendelea na ziara yake Bara la Ulaya kutafuta kuungwa mkono kuhusu kuiingilia kati kijeshi nchini Syria.
John Kerry akizungumza juu ya Syria akiwa Marekani
Hapo awali akiwa pamoja na mwenzake wa Ufaransa, Laurent Fabius, katika mkutano na waandishi wa habari, Bwana Kerry alisema kuwa nchi zaidi zinaunga mkono hatua ya kijeshi dhidi ya Syria kwa kutumia silaha za kemikali mwezi uliopita.
Ufaransa inaiunga mkono Marekani kuhusu Syria, lakini kama wanachama wengine wa Umoja wa Ulaya, inataka kusubiri ripoti ya wachunguzi wa silaha wa Umoja wa Mataifa waliozuru Syria.

Imewekwa na Happy Adam
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment