Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Saturday, September 7, 2013

Australia yamaliza kupiga kura

Raia wa Australia wamemaliza kupiga kura katika uchaguzi mkuu ambapo waziri mkuu wa chama cha Labor, Kevin Rudd, anakabiliwa na upinzani mkali kutoka kwa Tonny Abbott.
Wapihaji kura wa Australia wasubiri kwenye foleni
Kura za maoni za hivi karibuni zinaonesha Bwana Abbot na chama chake cha Liberal-National akiongoza, lakini wanasiasa wote wawili wanasema matokeo hayatabiriki na waliwaomba wafuasi wao wapige kura.
Foleni zilikuwa ndefu katika vituo vya kupiga kura - katika sheria ya Australia kupiga kura ni lazima kwa kila mtu zaidi ya umri wa miaka 18.
Maswala muhimu katika kampeni yalikuwa uchumi, wahamiaji na kodi juu ya uchafuzi wa mazingira.
Lakini katika kampeni wanasiasa wenyewe ndio walikuwa muhimu kushinda mjadala.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment