Writen by
sadataley
4:35 PM
-
0
Comments
Vita vikali vinaendelea kati ya wanajeshi, serikali na waasi, Mashariki mwa Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo.
Wapiganaji (Wanajeshi)
mmoja wa wanajeshi hao amesema kuwa kuwa ndege za kivita za serikali zimefanya mashambulio ya anga katika maeneo yao usiku ya kuamkia leo.
Umoja wa Mataifa kwa upande wake umesema uko tayari kutumia nguvu, kuwalinda raia ikiwa wapiganaji hao wa M23 wataingia mjini Goma.
Mapigano hayo yanatokea, huku jeshi la Umoja wa Mataifa litakalojumuisha wanajeshi elfu tatu likijiandaa kwenda eneo hilo kuwapokonya silaha wapiganaji wa waasi.
Mwaka uliopita waasi hao walijiondoa kutoka mji huo baada ya kuuteka kwa muda.
Mazungumzo ya amani kati ya wasi hao na wawakilishi wa serikali nchini Uganda yamekwama.
Raia wakikimbia makazi yao maeneo ya mashariki ya Kongo
Wakati huo huo, Mashirika ya kutoka misaada ya Kibinadam yamesema kuwa zaidi ya wakimbizi elfu sabini raia wa Congo wamekimbilia nchi jirani ya Uganda, kukwepa mapigano Mashariki mwa Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo.
No comments
Post a Comment