Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Monday, July 29, 2013

20 wauawa kwenye makabiliano Nigeria

 
Vijana hawa wanaungwa mkono na jeshi na hata wamepewa mafunzo kukabiliana na Boko Haram
Takriban watu 20 wameuawa nchini Nigeria baada ya makabiliano makali kati ya makundi ya vijana waliojihami na wapiganaji wa kiisilamu.
Hii ni kwa mujibu wa jeshi na vijana wanaotoa ulinzi kwa wanavijiji.
Kulingana na vijana hao wanaotoa ulinzi kwa niaba ya serikali, wapiganaji walivamia kijiji cha Dawashe kaskazini mwa nchi siku ya Jumamosi , kukabiliana na wapiganaji hao wa kiisilamu ambao nao walilipiza kisisasi kwa kutumia silaha nzito huku wakiwaua raia.
Kikundi hicho cha ulinzi kiliibuka mwezi Mei na kuanza harakati zake wakati huo.
Kimeahidi kusaidia serikali kupambana na wapiganaji wa Boko Haram.
Zaidi ya watu 2,000 wameuawa tangu mgogoro huu kuanza mwaka 2009.
Kundi la Boko Haram linasema kuwa linapigana dhidi ya serikali kutaka kuwa na utawala wa kiisilamu kote Nigeria.
Jeshi linatizama wapiganaji hao kama washirika wake na hivyo limewapa mafunzo kulisaidia katika harakati dhidi ya wapiganaji hao wa kiisialamu.
Kiongozi wa vijana hao Aliko Musa alisema kuwa watu 25 waliuawa mjini Dawashe katika jimbo la Borno ambalo ndilo kitovu cha harakati za Boko Haram.
Naye msemaji wa jeshi Haruna Mohammed Sani alithibitisha kuwa watu 20 waliuawa.

Chanzo:www.bbc.co.uk/swahili/habari/2013/07/130729_bokoharam_vigilante.shtml
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment