Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Saturday, June 29, 2013


KANISA LA KIINJILI LA KILUTHERI  TANZANIA 


DAYOSISI YA IRINGA 

"NAFASI YA KIJANA KATIKA KANISA".

SOMO LILOTOLEWA KATIKA KONGAMANO LA VIJANA  KATIKA USHARIKA  WA KIHESA 29-06-2013

Kanisa ni nini?
Kanisa  si jengo  tu bali ni wale waliomo ndani yake. Maana yake ya asili toka neno la Kiyunani ni ekklesia “kusanyiko”  "walioitwa" kama maneno katika msalaba ambao huwa ninauvaa. Neno Kanisa Iimo katika Biblia, Matendo ya mitume 17:24 "Mungu aliyeufanya ulimwengu na vitu vyote vilivyomo yeye kwa kuwa ni Bwana wa mbingu na nchi, hakai katika hekalu zilizojengwa kwa mikono."
Kanisa ni watu wanao amini Waefeso 2:21 "Katika yeye jengo lote linaungamanishwa vema na kukua hata liwe hekalu takatifu katika bwana." 1Wakorintho 3:16 "Hamjui ya kuwa ninyi mmekuwa hekalu la Mungu na yakuwa Roho wa Mungu anakaa ndani yenu?.
Kazi ya kanisa ni ipi? Kanisa linaeneza ijili  2 Timotheo 4:2 "Lihubiri neno uwe tayari wakati ufaao na wakati usiokufaa karipia kemea na kuonya kwa uvumilivu wote na mafundisho."
Kanisa limepewa maagizo na Mungu Waefeso 4:12 "Kwa kusudi kuwakamilisha watakatifu hata kazi ya huduma itendeke hata mwili wa Kristo ujengwe."
Kila mshiriki ana jukumu maalum 1 Wakorintho 12:13, "Kwa maana katika Roho mmoja sisi sote tulibatizwa kuwa mwili mmoja kwamba tu wayahudi au kwamba tu wayunani ikawa tu watumwa au ukawa tu huru nasi tulinyweshwa Roho mmoja."
Wakristo tu wafariji wenzetu Waebrania 10:25 "Wala tusiache kukusanyika pamoja kama ilivyo desturi ya wengine; bali tuonyane na kuzidi kufanya hivyo kwa kadiri muonavyo siku ile kuwa inakaribia.
Hivyo naenda kusema kuwa ndiyo sababu siku zote nikijitazama kama kijana humuona Mungu kuwa ni wa ajabu kuniumba hata mimi na kunifanya kuwa Mchungaji. Hivyo hukubaliana na nyimbo na waimbaji hawa ambao wamewahi sema kupitia nyimbo zao kuwa

a.            “Mungu wetu ndiye Boma”- Tumwabudu Mungu Wetu 302 na Dr. Martin Luther
Mungu ndiye ngao yetu na siraha yetu shetani akija kwetu tukiwa naye daima tutashinda na maadui zetu (shida,adha na changamoto za maisha yetu  yote). Tumtazame yeye kama Dr. Martin Luther alivyosema katika maneno ya wimbo wake huu. Anaimba wakati akiwa katikati ya mapambano na sisi tuimbe tunapopita katika hali mbalimbali katika maisha yetu.



b.            “Mungu ni Mwaminifu”. -Solomon Mkubwa
Mungu hatotuacha daima yeye hutunza maagano(makubaliano yetu nay eye) hivyo hata sisi tulivyo hapa anatujua na anaendelea kutunza uaminifu wake kwetu hivyo na sisi tusimame kwake tu, tumtazame yeye pekee.

c.            “Liseme kwani ni jambo usilolijua”- Sarah K
 kwani ni hakika hatuna tunalolijua katika maisha yetu ni yeye (Yesu) anatuwezesha ,ametuwezesha na ataendelea kutuwezesha.

d.            “I will be There, Just Call My name”. -Michael Jackson&Mariah Carey
Ipo siku tutaitwa kwenda Mbinguni na kila mmoja wetu ataitwa kwa jina lake; hivyo tujiandae.

e.            “Heri Kumjua Yesu Bwana”.  Tumwabudu Mungu Wetu 175 na F.J Crosby
Ni Yesu pekee atatuwezesha na kutuvusha na hata sasa anajua tulikotoka,tulipo na tuendako.

f.             “Msingi wa Kanisa Ndiye Yesu Bwana”. Tumwabudu Mungu Wetu 268 na samuel Stone
Kama tulivyoimba siku ile ya Kipaimara hebu tuendele kumtazama yesu kama msingi wa Kanisa na ndiyo njia pekee ya kutuvusha vijana, njooni tumtumikie kadili ya nafasi tunazojali. Tusiogope huku ni kuzuri tu hakuna shida yoyote.

LEO HII NAKUONA KIJANA MWENZANGU KAMA:-
  1. MSHARIKA MKAMILIFU ALIYEPO NA AJAYE

  1. KIONGOZI WA KANISA-MZEE WA KANISA-MTUMISHI WA MUNGU KADA MBALIMBALI


  1. MLEZI WA FAMILIA   AJAYE NA ALIYEPO (wajibu wako pale nyumbani kwa sasa).

  1. MZAZI AJAYE – (unayoyafanya sasa nawe utafanyiwa na m/watoto wako).
  2. MTETEZI WA WANYONGE (Haki za wanyonge na wanaonyanyaswa kuto kaa kimya kwani Dr. Martin Luther alisema utawajibika kwa yale uliyoyasema na usiyoyasema lakini ulipaswa kuyasema na umekaa kimya.)


  1. MWANA MAENDELEO ( Jiandae kuajili au kuleta mabadiliko katika eneo ambalo Mungu atakupa/amekupa).

A.    “Mkumbuke Muumba wako siku za ujana wako kabla hazijaja siku zilizo mbaya…” (Mhubiri12:1)

B.    “Nimewaandikia ninyi vijana, kwa sababu mna nguvu, na neno la Mungu  linakaa ndani  yenu, nanyi mmemshinda yule mwovu”.
             (I Yohana 2:14b).

C.   Na nimwibie mpenzi wangu wimbo wa mpenzi wangu katika habari za shamba lake la mzabibu. Mpenzi wangu alikuwa na shamba la mizabibu,kilimani penye kuzaa sana;akafanya handaki kulizunguka pande zote, akatwaa mawe yake,akapanda ndani yake mzabibu ulio mzuri, akajenga mnara katikati yake, akachimba shinikizo ndani yake;akatumaini ya kuwa utazaa zabibu, nao ukazaa zabibu-mwitu. Na sasa, enyi wenyeji wa yerusalem, namyi watu wa Yuda amueni, nawasihi mkato, kati ya mimi na shamba  langu la mizabibu….”(Isaya 5:1-7). 


UELEWA JUU YA UJANA NA KIJANA
1.     Ujana ni hatua ambayo mtu anaipitia baada ya utoto au ni kipindi cha kati cha makuzi ya mtu kabla ya utu uzima na hatimae uzee
2.    Ujana huanza mara baada ya mtu kubadilika kimaubile na huanzia miaka kumi na mbili wengine hadi kumi na tano ambapo mtu huanza kuwa na hisia za kimwili na kutamani sana kuwa na uhuru wake katika maamuzi. Mabadiliko haya huchochea au hupelekea hisia mbalimbali za kimwili na mabadiliko ya jumla ya tabia
3.    Ujana ni majira yanayopita katika makuzi ya mwanadu, ukifanikiwa kuwa mzee ni lazima ulipita katika kipindi hiki au daraja hili la ujana, kwa hiyo kama bado uko katika dara hili ni muhimu kujipanga ili usije ukajilaumu mbele ya safari
ZINGATIA HII
“Huwezi kuyajali maisha yako kama hujui thamani yake, huwezi kujua thamani ya maisha yako kama hujajitambua kwa Neno la Mungu, huwezi kuwa na maisha ya mafanikio kama maamuzi yako hayatengenezi mafanikio, ufahamu sahihi juu ya maisha yako ndio msingi wa kujitambua kwako, yaani kuijua Kweli ili hiyo Kweli ikuweke huru na ndipo utakapokuwa huru kweli kweli, kumbuka hata usipoamua maisha yako yataendelea kama kawaida. Zaidi ya hayo kama hujui wewe ni nani huwezi kujua thamani yako, kama hujui thamani yako lazima utaishi chini ya kiwango cha maisha unayotakiwa kuishi”.
UTAIJUAJE NAFASI YAKO KAMA KIJANA
Nafasi yako kama Kijana ni wajibu wako, umuhimu ulionao kwako na kwa jamii kwa ujumla wake pamoja na familia yako. Lazima ujue nafasi yako katika maeneo yafuatayo:
• Kwako binafsi,
• Katika familia yako,
• Kwa Kanisa lako,
• Kwa jamii yako
• kwa mkoa wako,
• kwa Taifa lako na
• kwa Ufalme wa Mungu.
Safari ya kujua nafasi yako katika maeneo yako hayo  hayo hapo juu  inaanzia katika eneo moja tu ambalo ni KUJITAMBUA
KUJITAMBUA NI NINI
“Kujitambua ni hali ya kuwa na ufahamu au uelewa (kujua) wa kutosha juu ya maisha yako kwa ujumla pamoja na mazingira yanayokuzunguka na hivyo kukufanya uishi maisha yanayofanana au kulingana na kusudi la Mungu kwako, uishi katika ubora wa maisha yanayolingana na kiwango cha ufahamu ulionao au kiwango cha kujitambua kwako kutegemeana na nguvu ya taarifa unazopata.
HIVYO BASI KIJANA ANATAKIWA  KUJUA KUWA:-
1. Kujitambua ni hatua ya muhimu katika maisha ya mtu yoyote duniani kama anataka kuishi kwa Furaha na matumaini na kufikia malengo yake
2. Kujitambua ni matokeo ya kupata ufahamu sahihi juu eneo fulani utakaokusaidia kufanya maamuzi sahihi katika eneo husika ili uweze kufanikiwa
3. Ufahamu au maarifa unapatikana kwa kutafuta, kuchunguza na kudadisi taarifa mbalimbali kwani si kila namna ya kujitambua ni sahihi kwa kijana
4. Matokeo ya ufahamu ulionao yatafanana na ubora wa maisha unayoishi kwa kiwango cha kuathiri maamuzi yako ya kila siku
5. Kiwango cha matokeo ya kujitambua kitafanana na ubora wa taarifa ulizozipata
6. Udhihirisho wa maisha ya kujitambau ni hatua ya juu kabisa ya kuthibitisha kwamba kweli umejitambua.
KUJITAMBUA NI LAZIMA KWANI:-
1. Ni lazima ujitambue, upate ufahamu sahihi juu ya maisha yako pamoja na mambo yote na jamii inayokuzunguka
2. Ni muhimu ujue wajibu ulionao kwako wewe mwenyewe kama mtu binafsi juu ya maisha yako
3. Kuna haja ya kujua kuwa wewe ni sehemu ya familia yako na lazima ujue wajibu wako kwa wazazi na familia kwa ujumla
4. Ni lazima ujifunze kuwa mzalendo wa taifa lako sawa na jinsi ambavyo Mungu anataka, fahamu kuwa umeunganishwa na ardhi ya Tanzania kwa mafanikio yako, Mungu akikwambia nenda nje ya nchi nenda lakini usifikiri mafanikio hayako Tanzania
5. Kijana unatakiwa ujitambue, ujielewe  kuwa wewe  ni nani na una kusudi gani katika maisha yako
6. Unatakiwa kupata uelewa wa kutosha juu ya kipindi cha ujana na umuhimu wake ukiwa bado Kijana ili ujue namna ya kuzingatia na kujipanga kwa hapo baadae
7. Kuelewa changamoto zilizopo katika kipindi cha ujana na namna ya kuzishinda kuna uhusiano na namna unavyojitambua ukiwa bado kijana
8. Kujenga shauku, nia na kiu kwa kijana ili aweze kuishi maisha yenye mwelekeo na aweze kutimiza maono yake akiwasaidia na wengine kumjua Mungu na maisha yake kwa ujumla wake
9. Kuwekeza uthamani na nguvu ya kipindi cha ujana kwa mtazamo wa Ufalme wa Mungu.
Imeandaliwa na
Mchg Kurwa Sadataley- Mratibu wa Idara
 Habari na Mawasiliano KKKT-DIRA


« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment