Writen by
sadataley
10:14 AM
-
0
Comments
BW. NAYMAN CHAVALLA: "HATUWEZI KUMALIZA TATIZO LA WATOTO WAISHIO KATIKA MAZINGIRA MAGUMU KUSINI MWA JANGWA LA SAHARA"
Bw. Nayman Chavalla Katibu Mkuu KKKT Dayosisi ya Iringa
Hayo yamesemwa na Katibu Mkuu wa KKKT,Dayosisi ya Iringa alipokuwa akizungumza na wageni marafiki wa kituo cha kulea watoto walio katika mazingira hatarishi( magumu) cha Huruma. Wageni hao wametoka Usharika wa Kilutheri Carvaly nchini Marekani,ambapo wamekuwa na mahusiano na kituo hicho tangu mwaka 1998. Kituo hicho ni maarufu kwa jina la Huruma Center ( Huruma Diaconical center) kinachomilikiwa na KKKT Dayosisi ya Iringa.
Pia Bw. Nayman Chavalla amewashukuru kwa kuendelea kukisaidia kituo na kuwaomba waendelee kufanya hivyo kwani kwa kufanya hivyo wanachangia katika kuubadilisha ulimwengu na kusaidia katika kuendeza juhudi za Kanisa katika kumsaidia mtu kamili yaani kiroho na kimwili.
Aidha amesema kituo cha Huruma kimebahatika kuwa na marafiki wa uhakika ambao ni Berlin Mission na Usharika wa Carvaly Lutheran toka Marekani. Na hakusita kusema pia wakati mwingine hupokea misaada mbalimbali toka St. Paul na sharika mbalimbali ili kuchangia huduma mbalimbali zinazohitajika katika kituo hicho.
Mama Constancia Chilewa Msimamizi wa Kituo
Profesa Gabriel K. Nzalayamisi Mwenyeji Mkazi wa Wageni
Mchungaji Sara Wirth toka Usharika wa Carvaly Lutherani Marekani
Katibu Mkuu akiwaelekeza juu ya mradi wa miti katika kitalu cha miti kilichopo makao makuu ya Dayosisi
Hapa wakiwa katika ofisi ya Waandishi wa redio Furaha 96.7 FM
Meneja wa Redio Furaha Bw. Protasi Kanemela akitoa maelezo huku Katibu Mkuu pembeni akimsikiliza kwa umakini mkubwa
Hapa wakiwa sehemu ya majadiliano
Hapa wakiwa katika Studio ya Redio Furaha
Mtangazaji Noel Kaguo
No comments
Post a Comment