Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Monday, May 20, 2013

KWAHERI MAMA MCHUNGAJI ANN KATRIN PERSSON



  Mama tunakushukuru sana kwa mapenzi mema ni maneo ya Baba askofu Dkt. O.M Mdegella wa K.K.K.T-Dayosisi ya Iringa
 "Hongeara mama" ni maneno ya Mchungaji Sara Mdegella kwa mama Ann Katrinn Person

  Mama Mchungaji Runne Persson katikati akiwa na baadhi ya watendakazi wenzake
      Hii ni zawadi yako Mungu akubariki sana
     Ubarikiwe sana 
      Nashukuru sana ni maneo ya mama Mchungaji Runne Persson

       Tunakutakia maisha mema na Mungu akipenda tutaonana


IFUATAYO NI SEHEMU YA HOTUBA YAKE 


Ninawashukuruni sana! Kwanza ninashukuru kwa jioni hii njema kwa ninyi nyote mliofika kwa kuniaga taja…, ni neema ya pekee. Ninashukuru mno! Halafu ninataka kusema asante kwa moyo na upendo mmenionyesha wakati nimekuwepo hapa Iringa, DIRA. Wengine nimekaa nao sana, na wengine tumeonana kwa kifupi tu. Lakini ninataka kusema kwamba ukaribu wenu pamoja na ukarimu umenitia moyo sana na imenisaidia kujisikia kama nipo nyumbani hapa, asanteni sana.
Wenzangu wa ETE, Mchg. Vallence, Mchg. Sarah, Mchg. Ulime na Mary, kama mimi ninavyoona tumefanya kazi vizuri pamoja. Tumepanga kazi,  tumezungumza, tumecheka na tumeomba pamoja ili kazi ya ETE isonge mbele na watu wapate nafasi kumfahamu Mungu wetu anayetaka watu wote wamfahamu  Yesu Kristo katika maisha yake.
Pia ninasema asante Sarah, kwa muda huu tuliokuwa pamoja ofisini na kwenye safari zetu za kuzunguka majimboni kuwaona wenzi wa wachg. na wainj. Umekuwa tayari kunieleza mambo yote ambayo sikuelewa na sikufahamu, na umekuwa tayari kunijibu kila swali. Hii imekuwa msaada mkubwa kwangu na imenisaidia sana katika kazi yangu. Sasa naomba Mungu akubariki katika kazi ya kuchunga Usharika wako, wenzi wa wachungaji na wainjilisti.
Miaka hii michache nimejifunza mengi kutoka kwenu. Na kitu kikubwa hasa ni maana ya maisha ya maombi.
Ninaporudi nyumbani nitaendelea kutoa habari za kazi ya wenzi katika usharika wetu ili wafadhili wenu wapate changamoto kuendelea kujitolea kwa kupitia SEM.
Muda umeenda haraka, miaka 2 ½ imeshapita, na sasa livu yangu imekwisha na nimeitwa kazini nyumbani tena. Mwakani Mungu akipenda, ninataka kufika hapa tena kumtembelea Rune na ninyi nyote, nafikiri Mungu anapenda.
Mungu awabariki ninyi nyote na tutaendelea kuwa pamoja katika maombi, asanteni sana!
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment