Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Sunday, May 19, 2013


WAZIRI MSTAAFU MH. FEDRICK T.SUMAYE AWAFUNDA WASOMI CHUO KIKUU IRINGA (THE IRINGA UNIVERSITY) ZAMANI TUMAINI UNIVERSITY-IRINGA  JUU YA UZALENDO AONYA VITA ZA KIDINI KUTIKISA TAIFA

HAYO AMEYASEMA ALIPOKUWA AKIONGOZA HARAMBEE YA UJENZI WA KANISA LA CHUO KIKUU HICHO . AMBAPO JUMLA YA  SHILINGI MILIONI  116,807,650 ZILIPATIKANA IKIWA  SHILINGI MILIONI  22,557,650 FEDHA TASLIMU  NA AHADI IKIWA NI SHILINGI MILIONI 94,250,000


 pichani Waziri Mkuu Mstaafu Mh. Fedrick T.Sumaye na Mkuu  wa Mkoa  wa Iringa Dkt Ishengoma  wakishiriki ibada kabla ya kuanza kwa harambee hiyo.
   Askofu wa KKKT Dayosisi ya  Iringa Dkt. Owdenburg Moses  Mdegella  na Msaidizi wake
 Mchungaji Blastone Gavile wakiongoza ibada kabla ya kuanza kwa harambee  hiyo
Mkuu wa chuo hicho akimuongoza mgeni rasmi katika ofisi yake tayari kwa kusaini kitabu cha wageni kabla ya kuanza  harambee  hiyo
  Katibu Mkuu Bw. Nayman Chavalla akifurahia jambo na Waziri Mkuu mstaafu Mh. Fredrick Sumaye

  Waziri Mkuu Mstaafu akisaini kitabu cha wageni
 Askofu wa KKKT Dayosisi ya  Iringa Dkt. Owdenburg Moses  Mdegella akikazia jambo kama sehemu ya maandalizi kabla ya kuanza kwa  harambee  hiyo 
Mkuu wa Chuo cha iringa Profesa Nicholaus Bangu akimuongoza Waziri Mkuu Mstaafu Mh. Fedrick T.Sumaye kuelekea kwenye mti aliopanda katika chuo hicho kama kumbukumbu yake mwaka 2002
 Askofu wa KKKT Dayosisi ya  Iringa Dkt. Owdenburg Moses  Mdegella akiteta jambo na Katibu mkuu wa Dayosisi Bw. nayman Chavalla
  Huu ndiyo mti uliopandwa na Mh. Waziri Mkuu Mstaafu mwaka 2002




  Viongozi waandamizi wa Dayosisi , Chuo wakiwa na Mkuu wa Mkoa wa Iringa  katika picha ya pamoja na Mgeni rasmi mbele ya mti huo
    Mchungaji Msigwa Mbunge wa Iringa Mjini akitoa salam zake katika harambee hiyo


   Mkuu wa Chuo cha iringa Profesa Nicholaus Bangu akitoa hotuba katika harambee hiyo

  Waandishi wa habari wakiwa katika kazi kulia ni Dada Tukuswiga Mwandishi wa Redio Furaha 96.7fm Fm 
   Kwaya  Kuu ya K.K.K.T-Dayosisi wakifuatilia hotuba ya mgeni rasmi kwa umakini mkubwa


Waziri Mkuu Mstaafu akisaini kitabu cha wageni

Askofu wa KKKT Dayosisi ya  Iringa Dkt. Owdenburg Moses  Mdegella ,Waziri Mkuu Mstaafu Mh. Fedrick T.Sumaye na Mkuu  wa Mkoa  wa Iringa Dkt Ishengoma  wakiwa katika harambee  hiyo

 Waziri Mkuu mstaafu, Frederick Sumaye akizungumza na  wasomi  wa chuo  cha Iringa


 

 Mbunge Msigwa akisalimia katika  harambee  hiyo huku  waziri mkuu mstaafu Bw Sumaye  wa nne  kulia kwake akimtazama

Mbunge Msigwa (kulia)akizungumza na msaidizi  wa Askofu Dean Blastone Gavile   
wa K.K.K.T Dayosisi ya Iringa 


 Mbunge  wa  jimbo la Iringa mjini mchungaji Peter Msigwa akiwa katika harambee ya ujenzi  wa Kanisa chuo  cha Iringa  ambako mgeni rasimi  ni Waziri Mkuu Mstaafu Frederick Sumaye 


          Mbunge Msigwa akisalimia katika harambee  iliyoendeshwa na Sumaye leo katika  chuo  cha  Iringa


 Waziri Mkuu mstaafu, Frederick Sumaye amewafunda  wasomi  wa  chuo  kikuu Iringa  zamani Tumaini  kuwa  watumie  kanisa  hilo litakalojengwa kwa ajili ya kueneza amani  zaidi  huku  akiwataka kuachana na masikitiko  yasiyo kwisha yanayotokana na  baadhi yao  kutojituma katika  kazi.
Sumaye  ametoa kauli  hiyo  leo katika  hotuba  yake kwa wasomi  wa chuo   kikuu cha Iringa kabla ya kuanza kuendesha harambee kwa ajili ya ujenzi  wa kanisa  la  chuo hicho.
Amesema  kuwa katika  Bibilia  rushwa na ufisadi ni  dhambi kubwa katika Taifa na  kuwa  vitu  hivyo  tunavilea wenyewe japo kuna tatizo  kubwa  na kuwa kaburi  pekee la mambo machafu ni  ujenzi  wa kanisa  hilo na matumizi yake  kutumika kwa malengo ya  kuhubiri amani na kukemea ufisadi.
" Mfano  ni nani kati yenu amepata  kutozwa  rushwa na mkulima ila rushwa  inatozwa na  wenye nafasi na hivyo lazima  vijana  wasomi  mkumaliza hapa lazima  kwenda  kubadilisha Taifa....ndio maana  nilipoitwa na baba  askofu kwa ajili ya changizo la kanisa nikasema nitafika kwani ni jambo jema"
Sumaye  alisema  kuwa kumshangilia  mtu anayeendesha gari la kifahari kwa  kulipata  kwa njia ya wizi ni hatari na kuendelea kuliangamiza Kanisani.
Alisema  kuwa  hivi  leo  watu  wanajenga  chuki kati ya  wanyonge na matajiri na  kuwa  hivi  sasa  limezuka jambo baya  zaidi kwa  watu kuchukiana kwa misingi ya  dini  zao na kuwa  nchi  yeyote  itakayoingia katika machafuko ya imani ni hatari  zaidi.
Sumaye  alisema  kuwa vita  ya kiimani ni mbaya  zaidi na siku  zote  vita  hiyo huwa haina mshindi  hivyo ni vema kila dini kuanza utaratibu  wa kuwafundisha  vijana  wake  ili  kuwa na uzalendo katika Taifa   hili.
Aidha  alisema  kuwa  mapambano ya  dini yanayoendelea  mbali ya kutokuwa na mshindi ila  bado  vita  hiyo haitakuwa na mshindi na  hivyo ni  vema  kila mmoja kuachwa akiendelea  kuamini kile ambacho ana amini  hata kama ni chini ya mti  asisumbuliwe.
Alisema  vita  ya  udini inayoendelea kwa   sasa  ni mbaya  zaidi  na  kuwa  watanzania  tusiruhusu vita   hiyo kupandikizwa .
Pia  alisema  kuwa  hivi  sasa  wapo baadhi ya  watu  wanaendelea  kuharibu Taifa  hili wakiwemo baadhi ya  watu  wanaoharibu  miundo  mbinu  ya barabara  kwa  kung'oa  vyuma  chakavu.
Waziri Sumaye  alisema kuwa  anafurahishwa zaidi kuona nyumba  za ibada  zinaendelea  kujengwa na  hivyo ni imani yake nyumba  za ibada  zitasaidia  kuhubiri amani na utulivu pamoja na uzalendo miongoni mwa watanzania.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment