Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Friday, February 15, 2013


RAIS KIKWETE ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU LAIZER ARUSHA

8E9U0677

Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete,Rais Mstaafu awamu ya Pili Mzee Ali Hassan Mwinyi,Rais Mstaafu awamu ya Tatu Benjamin William Mkapa na Waziri Mkuu Mstaafu Edward Lowassa wakishiriki ibada ya Mazishi ya Askofu Dkt.Thomas Laizer iliyofanyika katika kanisa na Usharika wa mjini Kati.mjini Arusha leo.

IMG_6518A
Rais Dkt,Jakaya Mrisho Kikwete akiteta jambo na Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu,Mh. Benjamin William Mkapa wakati wa Mazishi ya Askofu Thomas Laizer leo katika kanisa la KKKT Usharika wa mjini Kati
IMG_6373
Askofu Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT),Askofu Dk. Alex Malasusa akiongoza ibada ya Mazishi ya Askofu Thomas Laizer leo katika kanisa la KKKT Usharika wa mjini Kati,jijini Arusha
8E9U0890
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akiweka shada la Maua katika kaburi la Marehemu Askofu Dkt.Thomas Laizer wakati wa mazishi yaliyofanyika katika Kanisa KKKT Usharika wa mjini Kati,Arusha mjini leo.
Habari picha kwa hisani ya www.fullshangweblog.com 

JK ATOA HESHIMA ZA MWISHO KWA ASKOFU LAIZER

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete jioni ya jana, Alhamisi, Februari 14, 2013 ameungana na waumini wa Dayosisi ya Kaskazini Kati ya Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) kuuaga mwili wa Askofu wa Jimbo hilo, Askofu Dkt. Thomas Laizer.
Rais Kikwete na ujumbe wake amewasili kwenye Kanisa Kuu la KKKT mjini Arusha kiasi cha saa 10:50 akaenda moja kwa moja kuaga mwili wa Marehemu Laizer na baadaye akakuta na kuwafariji wafiwa akiwamo Mke wa Askofu Laizer, Mama Maria Laizer.
Rais pia atashiriki mazishi yake yaliyopangwa kufanyika kesho, Ijumaa, Februari 15, 2013 katika Kanisa Kuu hilo la KKKT la mjini Arusha.
Askofu Dkt. Thomas Olmorijoi Laizer ambaye alizaliwa Machi 10, mwaka 1945 katika Kijiji cha Engarenaibor, Wilaya ya Longido, Mkoa wa Arusha alifariki dunia Alhamisi iliyopita, Februari 7, majita ya saa 12 jioni kwa magonjwa ya Kisukari na Shinikizo la Damu.

Habari kwa hisani ya Mjengwa Blog


                         Picha kwa hisani ya bashir-nkoromo.blogspot.com

JK AONGOZA MAELFU MAZISHI YA ASKOFU MSARIKIE

RAIS Jakaya Kikwete, jana aliongoza maelfu ya waumini wa Kanisa Katoliki Jimbo la Moshi, mkoani Kilimanjaro, wananchi na wageni kutoka ndani na nje ya nchi, katika mazishi ya aliyekuwa Askofu mstaafu wa kanisa hilo jimbo la Moshi, Amedius Msarikie (82).

Mazishi hayo yalifanyika katika Kanisa Kuu la Kristu Mfalme, mjini humo ambapo katika salamu zake, Rais Kikwete alisema marehemu alipenda maendeleo, kusimama na kushiriki kwa vitendo katika mambo mbalimbali ambayo aliyaamini.

“Askofu Msarikie alianzisha Chuo Kikuu kinachotoa mafunzo
kwa walimu wa sayansi eneo ambalo Serikali inahitaji kubwa,
hii ni kazi nzuri ambayo haina budi kuigwa na kuendelezwa,” alisema Rais Kikwete na kuongeza kuwa, Serikali itaendeleza
juhudi zote alizoanzisha ili kuchochea maendeleo zaidi.

Alisema marehemu alikuwa muumini mkubwa wa amani, upendo
na mshauri mzuri katika mambo mbalimbali ambayo yatamfanya aendelee kukumbukwa siku hadi siku.
    Rais akitoa heshima za mwisho 
              Rais akiweka shada la maua
    Rais akiweka mchanga katika kaburi la Askofu

Picha zote  kwa hisani ya kajunason.blog
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment