Latest News

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)

UNIVERSITY OF IRINGA (Formerly Tumaini University-Iringa)
CALL FOR MARCH INTAKE APPLICATION 2017/18
NOW OPEN!
DEADLINE 30/03/2018
CALL 0743 802 615, 0677 048 677Read More

menu

Saturday, March 17, 2018

KWANINI KICHUYA AMEANZIA BENCHI LEO; KOCHA LECHANTRE HUYU HAPA AKIFAFANUA.



Baada ya kikosi cha Simba kinachoivaa Al Masry katika mechi ya Kombe la Shirikisho kuonekana kumekuwa na mjadala mkubwa kuhusiana na kuanzia benchi kwa kiungo Shiza Kichuya.

Simba inaivaa Al Masry hapa POrt Said katika mechi ya Kombe la Shirikisho. Mechi ya kwanza imeisha kwa sare ya 2-2.

Kocha Pierre Lechantre ameonekana kuelewa vizuri kwa nini ameamua Kichuya aanzie nje.

Lechantre amesema Kichuya ana nafasi ya kuingia baadaye kwa kuwa mfumo atakaoanza nao si ule unamruhusu Kichuya kuanza.

“Al Masry ina wachezaji wengi wenye ubora, nimeangalia mechi zao nyingi sana. Najua wanacheza vipi.

“Kipindi cha kwanza lazima tukabe sana na kuhakikisha tunaziba njia zote. Kichuya ni mzuri mnapokuwa mnashambulia, mkiwa na mpira.

“Mnapopoteza mpira, anakuwa chini sana. Sasa mwanzo tunahitaji mtu mzuri hata mnapokuwa hamna mpira na Kotei anaweza kukaba.

“Kichua ana nafasi ya kuingia na hasa dakika thelathini za mwisho ambazo tutahitaji kushambulia zaidi,” alisema.

Awali ilionekana kuwa na maswali mengi kuhusiana na Kichuya kuanzia katika benchi katika ngumu dhidi ya Al Masry. Baada ya dakika kumi kutoka sasa, Simba wataanza safari kutoka hotelini kwenda uwanjani.
« PREV
NEXT »

No comments

Post a Comment