Writen by
sadataley
6:48 PM
-
0
Comments
Bunge la Somalia limeidhinisha uteuzi wa Hassan Ali Kheyra kuwa waziri mkuu.
Kheyra
ambaye aliwahi kufanya kazi kama mshauri na mkurugeni mkuu wa kampuni
ya mafuta anatarajiwa kuteua baraza lake la mawaziri.Akihutubia bunge, alisema kuwa lengo lake kuu ni kukabiliana na ukame uliopo, kuimarisha usalama mbali na kukabiliana na ufisadi.
Hatahivyo kazi ya mkuu huyo wa serikali ya Somalia huenda ikapungua baada ya Umoja wa Mataifa kuonya kwamba Somalia ipo katika hatari ya kukumbwa na baa la njaa pamoja na tishio la usalama linalotolewa na kundi la wapiganaji wa al-Shabab.
No comments
Post a Comment