Writen by
sadataley
6:44 PM
-
0
Comments
Blackman na bintiye Christabel mwaka 2005
Michoro hiyo ya Charles Blackman inayojulikana kama Women Lovers, inaonyesha wanawake wawili walio uchi ambao wako kitandani kando mwa paka.
Muuza michoro Mossgreen, alijaribu kuutangaza mchoro huo kupitia kwa Facebook lakini mtandao huo uliukataa.
Mkurugenzi mkuu wa Mossgreen Paul Summer, anaitaja hatua hiyo ya Facebook kama ya kushangaza.
Facebook inasema kuwa uamuzi wake ndio wa mwisho lakini Mossgreen wameichapisha tena michoro hiyo.
Mwezi uiopita mwalimu mmoja nchini Ufaransa aliushtaki mtandao wa Facebook, kwa kufuta ukurasa wake baada ya kuchapisha picha ya utupu ya mwanamke iliyochorwa karne ya 19.
Bwana Summer anasema mchoro huo wa Women Lovers, ulitarajiwa kuuzwa kwa zaidi ya dola 34,000 wiki ijayo.
Chanzo:Muungwana Blog
No comments
Post a Comment